WAZIRI MKUU MAJALIWA AKAGUA VIWANJA VYA MAZOEZI CHAN 2025


Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amefanya ukaguzi wa viwanja vitakavyotumiwa kufanyia mazoezi na timu zitakazoshiriki michuano ya kombe la Afrika kwa Wachezaji wa Ligi za ndani (CHAN) mwaka huu na Kombe la mataifa Afrika (AFCON) mwaka 2027.

Majaliwa alifanya ukaguzi huo Machi 29,2025 Jijijini Dar es Salaamkatika viwanja vya Gymkhana. Meja Jenerali Isamuhyo na kiwanja cha Chuo cha Sheria (Law School), vyote vilivyopo jijini Dar es Salaam.

Michuano ya CHAN  inayotarajiwa kuffanyika Agosti mwaka huu na AFCON mwaka 2027 , itapigwa katika nchi za Tanzania, Kenya na Uganda.

Baada ya ukaguzi huo, Waziri Mkuu Majaliwa aliwaagiza Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, na Katibu Mkuu Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa kushirikiana na KAtibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu (TFF) kufanya tathmini ya kazi ya ujenzi na ukarabati wa viwanja vya mazoezi  vitakavyotumika kwenye michuano hiyo.

Alitoa maelekezo hayo baada ya kupokea maelezo kutoka kwa Mkurugenzi mtendaji wa SUMA JKT Brigedia Jenerali Petro Ngata ambaye  ndiyo Wakandarasi wa mradi huo.

Majaliwa alisema ni vyema ufuatiliaji wa karibu wa kila hatua za ujenzi na ukarabati ukafanyika ikiwa ni pamoja na ukaguzi wa vifaa vyote ambavyo Mkurugenzi huyo amesema tayari vuimenunuliwa na viko stoo.

Awali, Brigedia Jenerali Ngata , alimueleza Waziri Mkuu kuwa; kwa ujumla ujenzi na ukarabati umefikia asilimia 80 ya kazi kwa viwanja vyote ambavyo ni pamoja na ujenzi wa sehemu ya kuchezea (pitch), vyumba vya wachezaji  pamoja na majukwaa.

Michuano ya Kombe la Afrika (CHAN) inayoshirikisha Wachezaji wa ndani inatarajiwa kufanyika kuanzia Agosti 2 hadi 30 mwaka huu baada ya kuahirishwa  mwaka 2024 huku michuano ya Kombe la Mataifa Afrika (AFCON) yanatarajiwa kufanyika mwaka 2027.

 


Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.