MWEKA-KILIMANJARO.
Timu
ya Wafanyakazi wa Benki ya NMB wamefanikiwa Kuifikisha Tuzo ya Mwajiri Kinara, katika
kilele cha Mlima Kilimanjaro.
Akizungumza
katika hafla ya mapokezi iliyofanyika katika lango la Mweka, Mkuu wa Idara ya Rasilimali Watu NMB
Jeseph Ngalawa, aliishukuru timu hiyo kuwa kuweza kuifikisha bendera na Tuzo hiyo,
ambayo walikabidhiwa kama Mwajiri Kinara Tanzania.
Alisema
ili uweze kupanda mlima Kilimanjaro inahitaji ustahimilivu wa hali ya juu,
ushirikiano wa dhati na dhamira thabiti hivi ndio vitu ambavyo vinahitajika pia
hata katika utekelezaji wa majakumu kama
Benki ya NBM na ndio vitu ambavyo vimepelekea Benki ya NBM kutambukila kama Mwajiri
bora hapa nchini.
Alisema
Benki ya NMB waliona ni jambo zuri
kuipeleka Tuzo hiyo Mlima Kilimanjaro, kwa sababu ni Mlima unaotambuliwa
Kimataifa.
Akizungumza
kiongozi wa waliopandisha bendera na Tuzo ya Mwajiri Kinara Meneja wa NMB
Ngalenaro Limbris Israel, alisema jumla ya watu wanne waliopanda mlima huo wote
wamefanikiwa kufika katika kilele cha mlima Kiliamnajro.
Akizungumzia
changamoto ya kuupanda mlima huo Israel alisema; baadhi ya watu wengi wanahofu
kubwa ya kuupanda mlima huo mrefu barani afrika kutoka na kupewa historia za
mlima wenyewe kwa jinsi ulivyo.
Naye Afisa Masoko kutoka Kampuni ya utalii “Zara tours Adventure” Nance Ngotea; aliishukuru Benki ya NMB kwa kuichagua kampuni hiyo kuweza kuwapandisha wafanyakazi hao.