Wananchi wasisitizwa kuitumia wiki ya sheria kama fursa

Wakili wa Serikali Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali  Mkoa wa Kilimanjaro Tamari Mndeme, akizungumza na Waandishi wa Habari ofisini kwake kuelekea uzinduzi wa Kamati ya Ushauri wa Kisheria, hafla itakayofanyika Januaria 21, 2025.

MOSHI-KILIMANJARO

Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Nurdin Babu, anatarajiwa kuzindua  Kamati ya Ushauri wa Kisheria, huku wananchi wakitakiwa kuhakikisha wanafika katika kliniki hiyo na kupata elimu ya sheria ili itakayotolewa bure kwa kipindi cha wiki moja kuanzia Januari 21hadi  januari 27 mwaka huu.

Mwenyekiti wa Kamati ya Ushauri wa Kisheria  mkoa wa Kilimanjaro Tamari Mndeme, aliyasema hayo Januari 19, 2025 wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisni kwake.

Alisema baada ya kuzinduliwa kwa Kamati hiyo kwa kushirikiana na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali,  Kamati hiyo itaanza rasmi kazi ya kuendesha kliniki hiyo, ambayo itakuwa imesheheni maofisa kutoka taasisi mbalimbali za serikali.

“Kliniki hii itafanyika kuanzia Januari 21, mwaka huu katika viwanja vya stendi kuu ya mabasi Moshi, nawashauri wananchi  kuitumia fursa hii adhimu ili waweze kuja kupata ushauri wa kisheria ambao utawasaidia kutatuliwa kwa changamoto zao,”alisema.

Mndeme ambaye pia ni Wakili wa Serikali Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali  mkoani humo, alisema wananchi wamekuwa na malalamiko na migogoro mingi inayohusu mambo ya kisheria na hawajui sheria na kuwataka kuitumia wiki hiyo ya sheria.

“Kesi nyingi zinazowasilishwa na wananchiwa mkoani humo, zinahusiana na masuala ya ardhi, mirathi, ukatili, ndoa na masuala mengine ya kijamii.”alisema.

Katibu wa Kamati ya Ushauri wa Kisheria mkoa wa Kilimanjaro, Kisa Lyimo, alisema programu ya msaada wa kisheria, imeanzishwa kwa madhumuni ya kuwasaidia wananchi kupunguza migogoro na malalamiko ya kisheria yanayowakabili.

Nao baadhi ya wakazi wa Manispaa ya Moshi Msumari Simoni, Adam Seif na Mwl Japhet Mpande, walisema ujio wa kliniki hiyo utawasaidia kuwatatulia changamoto zinazowakabili ikiwemo migogoro ya ardhi.

Timu ya Waandishi wa Habari mkoa wa Kilimanjaro wakiwa katika mkutano na Wakili wa Serikali Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali  Mkoa wa Kilimanjaro Tamari Mndeme hayupo katika picha, kuzungumzia uzinduzi wa  Kamati ya Ushauri wa Kisheria, inayotarajiwa kufanyika Januaria 21, 2025.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.