Sh bilioni 1. kutumika kujenga Chuo cha Uuguzi Rombo

ROMBO-KILIMANJARO.

Serikali kupitia Wizara ya Afya imetenga fedha Sh bilioni 1 katika Bajeti ya Mwaka 2024/25 kwa ajili ya kujenga chuo  cha uuguzi Wilayani Rombo mkoani Kilimanjaro.

Waziri wa Afya Jenista Mhagama aliyasema hayo Januari 7,2025 Wilayani Rombo, wakati akiwa katika ziara ya siku mbili mkoani Kilimanjaro, kwa lengo la kukagua na kuzindua miradi ya Sekta ya Afya katika Wilaya ya Rombo pamoja na Wilaya ya Same.

Alisema Serikali imetenga zaidi ya Sh bilioni 1 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa chuo hicho, ambacho kitajengwa  wilayani Rombo, ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Makamu wa Rais Dk. Philip Mpango.

Waziri Mhagama, alisema ujenzi huo unaratajiwa kuanza mwezi Machi mwaka huu, ili kupunguza tatizo la watumishi wa kada ya afya na chuo hicho kitakuwa na uwezo wa kuchukua vijana takribani 600 huku vijana watakao kuwa wakiishi kwenye mabweni ni 400.

“Serikali imeona ipo haja ya kuongeza idadi ya wataalam wa Afya kwa kujenga Chuo cha uuguzi ili kuboresha upatikanaji wa wataalam wa afya nchini.”alisema Waziri Mhagama.

Aidha Waziri Mhagama, alisema ndani ya miaka mitatu ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan Serikali ilitoa Sh bilioni 82 katika Wilaya Rombo, ili kutekeleza miradi mbalimbali ikiwemo miradi ya afya.

Kwa upande wake Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Nurdin Babu, aliishukuru Serikali huku akisema kuwa katika kipindi cha miaka mitatu ra Rais Samia madarakani, mkoa ulipokea Sh bilioni 956 za miradi ya maendeleo.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.