Wawekezaji waalikwa kujenga hoteli zenye hadhi hifadhi ya Mkomazi

MOSHI-KILIMANJARO.

Mkuu wa Wilaya ya Same Kaslida Jeremiah Mgeni, amewaalika wawekezaji kuja kuwekeza kwenye Sekta ya Utalii kwa kujenga hoteli zenye hadhi.

Hatua hiyo inakuja kutokana na  Wilaya hiyo kuwa na wageni wengi wanaokuja kutembelea, Hifadhi ya Taifa ya Mkomazi, kupitia mradi wa  Mbwa mwitu na Faru ndani ya hifadhi hiyo ambao umefanya idadi ya wageni kuongezeka kwa asilimia 100 kwa mwaka.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini Moshi, kuhusiana na Tamasha kubwa linalojulikana kama “Same Utalii Festival” ambapo tamasha hilo litafanyika Disemba 20 hadi 22 mwaka huu.

Kasilda amesema kukosekana kwa hoteli zenye hadhi, baadhi ya watalii wanalazimika kwenda kulala Moshi, kutokana na ukosefu wa hoteli zenye viwango na kutoa rai kwa wafanyabiashara kuja kuwekeza kwa kujenga hoteli zenye hadhi ili watalii wanapokuja kutembelea hifadhi hiyo wasipate adha ya kupata mahali pa kulala.

Amesema tangu kuanzishwa kwa Tamasha la Same Utalii Festival, wawekezaji wamehamasika kuja kuwekeza kwa kujenga hoteli zenye hadhi, ambapo mwekezaji mmoja amejenga hoteli kwenye lango la kuelekea Mkomazai huku hoteli mbli zikijengwa kwenye mlima wa hifadhi ya Shengena moja wapo ikiwa ya nyota tano.

 “Tamasha la Utalii Festival, imekuwa na tija kubwa, limeongeza ajira kwa vijana, hoteli zinazojengwa ajira zitaongezeka, waongoza watalii wengi wataongezeka, kupitia vivutio vya utalii ulivyoko wilaya kwetu.”amesema.

Aidha amesema idadi ya watalii wanaotembelea Hifadhi ya Taifa ya Mkomazi imeongezeka ambapo kwa mwaka 2023 takribani watalii 7,000 walitembele hifadhi hiyo na kwamba baada ya tamasha hili kufanyika idadi imeongezeka na kufikia watalii 10,000.

“Baada  Tamasha la Utalii Festival-one,  hadi sasa  idadi ya watalii imeongezeka  kutoka watalii 7000 hadi kufikia watalii 10,000 jambo ambalo limeleta matumaini makubwa sana kwa wananchi wa Same,

Ameongeza ”Kuwepo kwa mradi wa Mbwa mwitu na Faru,  imekuwa ni kivutio kikubwa cha utalii, hususan watalii kutoka nje ya nchini, ambao wamekuwa wakitembelea hifadhi hiyo kutokana na  uwepo  wa vivutio hivyo.”amesema.







Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.