Wananchi watakiwa kuchangamkia fursa za kiuchumi kupitia utalii

MWANGA-KILIMANJARO.

Serikali mkoa wa Kilimanjaro, imewataka Wananchi mkoa huo, kuchangamkia fursa za kiuchumi zinazotokana na sekta ya utalii zilizopo katika maeneo yao kwa kufanya biashara mbalimbali ili kuendeleza uchumi wao na wa mkoa kwa ujumla.

Hayo yamesemwa jana na Katibu Tawala mkoa huo,  Kiseo Nzowa, katika hafla ya uzinduzi wa Tamasha la Mwanga na Mbio za Mwanga Marathon zilizofanyika desemba 27,2024  Wilayani humo katika viwanja vya CM Msuya.

Nzowa alisisitiza umuhimu wa utalii katika kukuza ajira na biashara na kuwahimiza wananchi wa wilaya hiyo, kutafuta njia za kuunganishwa na sekta hiyo ili wawezae kunufaika na fursa zilizopo.

Aidha aliutaka uongozi wa Wilaya hiyo kuhakikisha kwamba wanavitangaza vivutio vya utalii vilivyopo ili kuvutia wawekezaji wengi kuja kuwekeza ndani ya wilaya hiyo

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Mwanga Mwanahamisi Mnkunda, ameitaka Wakala wa Barabara Vijijini na Mijini (TARURA) kuharakisha ujenzi wa barabara ya Karamba ndea, kuelekea lango la hifadhi ya Taifa ya Mkomazi na hivyo kukuza utalii na mapato ya halmashauri kwa ujumla

Aidha alisema serikali wilayani humo, imejipanga, kuhakikisha kwamba maeneo yote yenye vivutio vya utalii wanakwenda kuyalinda ili kuchochea Uchumi, pamoja na kuwakaribisha wawelezaji wa ndani, kuja kuwekeza katika sekta ya utalii.

Munkunda alisema Wilaya hiyo ina malengo ya kuanzisha kituo kidogo cha forodha, kupitia lango hilo, ili kusaidia watalii wanaotoka hifadhi ya Taifa Tsavo nchini Kenya, waweze kupata huduma za kiforodha ndani ya lango hilo.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Mwanga Joseph Tadayo, alisema toka serikali ya awamu ya sita kuingia madarakani, imerudisha ule mfumo wa ushirikiano kati ya sekta binafsi na sekya ya umma, jambo ambalo limewezesha kuweko kwa maendeleo makubwa ndani ya wilaya hiyo.

Akizungumza kwa nyakati tofauti, Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kupitia mkoa wa Kilimanjaro, Seleman Mfinanga na Mkuu wa Wilaya ya Tanga Japhari Kubecha,   ambao ni wazaliwa wa wilaya hiyo, walimpongeza Mkuu wa  Wilaya ya Mwanga Mwanahamisi Munkunda, kwa kuja na wazo la kuanzisha mbio hizo ambazo zimewakutanisha Wanadiaspora na kuweza kukaa  kwa pamoja na kuweza kufahamiana.













Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.