Ukuaji wa matamasha ya utalii kuchochea maendeleo ya utamaduni nchini

SAME-KILIMANJARO.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Methusela Ntonda, amesema kwamba ukuaji wa matamasha ya utamaduni utachochea maendeleo ya sekta ya Utalii, na hivyo kuvutia watalii wengi kutembelea vivutio mbalimbali nchini.

Akitoa salamu za Waziri wa Wizara hiyo kwenye ufunguzi wa Tamasha la Utalii Same, Ntonda amesema kuwa tamasha hilo litachangia kukuza utalii wa ndani na nje ya nchi na pia litasaidia kutangaza na kuhifadhi utamaduni, mila na desturi za watu wa wilaya ya Same.

Ntonda amesema ukuaji wa matamasha ya utalii, yatasaidia kuimarisha sekta ya utalii kwa manufaa ya taifa, jambo ambalo litasaidia kukuza utamaduni, mila na desturi za taifa kuweza kudumishwa zaidi.

“Ukuaji wa tamasha hili utachochea kuvutia utalii wa taifa na pia kuendelea kutangaza utamaduni, mila na desturi za watu wa same, na hivyo kuweka utamaduni wa taifa kuwa endelevu na kuimarisha masula ya utalii,”amesema Ntonda.

Pia amempongeza mkuu wa wilaya ya Same kwa kuja na wazo la kuvitangaza vivutio vya utalii  vilivyopo katika wilaya hiyo, na kwamba kama Wizara itaendelea kufungamanisha utalii na utamaduni katika matamasha hayo.

“Naishukuru Kamati ya maandalizi kwa kutafsiri vyema maono ya Rais Samia, katika sekta ya utalii kwani kupitia tamasha hili tumeshuhudia shughuli mbalimbali zinazofanyika zikiwemo shughuli za utamaduni na michezo, hivyo Wizara itaendelea kushirikiana na waratibu wa matamasha haya ili kuwa karibu zaidi ili kuweza kufikia makundi yote hususani watoto wadogo, ambao ndio lengo kuu la Wizara katika kuwarithisha utamaduni.”amesema.

Aidha amevisistiza vitengo vya idara katika Wizara hiyo, kuhakikisha mazao ya matamasha haya yanabuniwa ili kuweza kuwa vivutio vikubwa katika katika tasnia hiyo.

Katika Tamasha la Utalii Same awamu ya pili, Waziri wa Maliasili na Utalii Balozi Dk. Pindi Chana, utoa tunzo mbalimbali kwa wadau ili kutambua mchango wao katika kufanikisha tamasha hilo.











Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.