HAI-KILIMANJARO
Mkuu wa Mkoa wa
Kilimanjaro Nurdin Babu, amesema Serikali imedhamiria kuona Tanzania inakuwa na
viongozi wa kimila, wanaoisaidia Serikali katika kutatua changamoto zilizoko
kwenye jamii.
Aidha amesema
viongozi wa kimila, wana msaada mkubwa katika kuelimisha na kufundisha juu ya
kuongoza jamii, kuonya na kuwaadhibu wanaokwenda kinyume na maadili.
Akiwa mgeni rasmi
katika tukio la kupandishwa daraja Mangi mkuu wa Machame Gilbert Gilead
Shangali, Babu amesema, mkoa wa Kilimanjaro uko mstari wa mbele kulinda
na kudumisha mila na desturi za kiafrika.
"Mimi sitakasirika, wala sitashangaa kama mkichukua hatua kwa mujibu wa taratibu zenu za kimila, matarajio yetu kama Serikali ya mkoa ni kuhakikisha nidhamu iliyopotea inarejeshwa,"amesema RC Babu.
Amesema
kwa sasa Tanzania, imeingioa katika wimbi kubwa la vitendo vya ulawiti na ushoga,
huku akitoa rai kwa Watanzania na wana Kilimanjaro kwa ujumla, kutokupenda
kujiingiza kwenye mambo ambayo hawakuzaliwa nayo, kuiga utamaduni wa nchi
za magharibi kutawaharibu watoto."
"Jamii
imekumbwa na tatizo la mmomonyoko wa maadili, maendeleo ya Teknolojia hasa
katika upande wa mawasiliano, yamesababisha athari na kumuomba Mangi Gilbert
Gilead Shangali, kuhakikisha anasimamia maadili ikiwa ni pamoja na vijana
wanaolewa pombe nyakati za asubuhi wapewe adhabu kali,"amesema.
Naye Katibu Tawala
mkoa huo Kiseo Nzowa, amempongeza Mangi Gilbert Gilead Shangali, kwa kutawazwa
kuwa Mangi wa Machame.
"Nitoe pongezi
zangu za dhati kabisa kwa ndugu yetu
Gilbert Gilead Shangali, kwa kutawazwa
kwako kuwa Mangi ,ukiwa kiongozi mwenzetu wa kijamii, sote ni viongozi wa
kuwaongoza Wanannchi , tunakuahidi kama Serikali kukupa ushirikiano wa kila
namna, utakaohitajika ili kuyafanya majukumu yao kuwa mepesi,"amesema
Nzowa.
Mwenyekiti wa Jumuiya
ya Amani na Maridhiano Tanzania (JMT), mkoa huo, Askofu Jones Mola, amesema
viongozi wa kimila wana mchango wa kipekee katika kujenga taifa lenye
mshikamano, amani, utulivu na kuchangia katika maendeleo endelevu
yanayozingatia urithi wa kitamaduni na maadili ya taifa.
Naye Sheikh wa mkoa
wa Kilimanjaro Shaban Mlewa, amesema kiongozi akiwa ni mtu mwenye tamaa,
atawafanya hata anaowaongoza kuwa na tama na kumsihi Mangi Gilbert Gilead
Shangali kutokujiingiza na vitendo hivyo.
.jpg)

.jpg)




.jpg)
