Manispaa ya Moshi yamshukuru Rais Samia kwa kwapandisha madaraja watumishi 1000, ajira mpya 54, kupandisha vyeo watumishi 61

MANISPAA-MOSHI

Halmashauri ya Manispaa ya Moshi, mkoa wa Kilimanjaro, imemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan, kwa kuwapandisha madaraja Watumisi zaidi ya 1000 na kuwalipa malimbikizo yao ya mishahara.

Taarifa ya Serikali kuhusu kupandishwa madaraja watumishi na kuwalipa malimbikizo ya mishahara, imetolewa jana na Mkurugenzi mtendahi wa Manispaa hiyo Mwl. Mwajuma Nasombe, wakati akizungumza na Watumishi wa Manispaa hiyo.

Amesema katika kipindi cha mwaka wa fedha 2024/2025 Rais Samia ameruhusu, upandishwaji wa vyeo kwa watumishi 1,071, ajira mpya 54 na kubadilishwa vyeo watumishi 61.

“Sisi watumishi wa Manispaa ya Moshi, tunamshukuru sana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan, kwa kuwapatandisha madaraja watumishi zaidi ya 1, 000  kwa kipindi akiwa madarakani, pia tunamshukuru kwa kuleta ajira mpya 54 ndani ya Manispaa yetu ya  Moshi , kubadilisha vyeo watumishi 61 ambapo huko nyuma ilikuwa njozi na sasa chini ya Rais  Dk. Samia imewezekana.”amesema Mwl. Nsombe.

Mwl. Nasombe amesema Serikali kuwapatia stahiki zao, inataongezea watumishi  morali ya kufanya kazi na kuondoa manung’uniko na visingizio vya viporo kazini, huku akiwataka watumishi hao kufanya kazi kwa ari zaidi ili kuifanya Manispaa iendelee kupiga hatua zaidi.

Aidha Mkurugenzi huyo, amepiga  marufuku kwa mtumishi yeyote wa umma, kufika kazini akiwa amelewa au  kutumia vilevi wakati wa kazi, na kwamba hatua kali zitachukuliwa dhidi ya wahusika, ikiwa ni pamoja na kuondolewa kazini.

Mwl.  Nasombe, ameyataja  matumizi ya vilevi kazini ni mojawapo ya mifano ya utovu wa nidhamu, huku akisema kuwa ni aibu kwa mtumishi wa umma ambaye anadhihirisha tabia za kulewa, huku akieleza kuwa nidhamu ni nguzo muhimu ya mafanikio katika utendaji kazi.

“Nidhamu, inahusisha pia kuheshimu taratibu, viongozi, na wenzao kazini, uzembe, tabia mbaya, na uvunjifu wa maadili ni baadhi ya mifano ya utovu wa nidhamu, ambayo inaweza kusababisha kuvunjwa kwa kanuni za kudumu za utumishi wa umma za mwaka 2009.”amesema.

Mkurugenzi huyo, pia aliwataka watumishi wa halmashauri ya Manispaa hiyo, kufanya kazi kwa kushirikiana na kusaidiana ili kazi katika idara ziweze kufanyika kwa ufanisi.

Akizungumzia suala la uwajibikaji Mwl. Nasombe, amesema ni moyo wa utendaji bora, ambapo kila kila mmoja ana jukumu la kuhakikisha anatimiza majukumu yake kwa uaminifu na weledi.

“Serikali ilianzisha mfumo wa upimaji, utendaji kazi kwa watumishi na upimaji wa taasisi (PEPMIS) ambayo sasa inajulikana kama mfumo wa e-Utendaji, ili kila mtumishi aweze kuingiza mipango yake ya kazi na kisha kutoa taarifa za utendaji wa kazi hizo kwenye mfumo, kulingana na mpango ambao kila mtumishi ameingia.

Ameongeza kuwa “Jambo la kusikitisha ni kwamba amepokea orodha ya watumishi ishirini na nane (28) ambao hadi sasa hawajaingiza mpango wao wa kazi katika mfumo huo kwa mwaka wa fedha 2024/2025, watumishi hao wameshindwa kuwajibika kwa kutotii maelekezo ya serikali na wanastahili kuchukuliwa hatua za kinidhamu kwa kuvunja kanuni za utumishi wa umma za mwaka 2022 kanuni 42 (8) ikisomwa pamoja na kanuni za kudumu za utumishi wa umma za mwaka 2009.

Nao baadhi ya watumishi wa halmashauri hiyo, wamemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan, kwa kuwapandisha madaraja watumishi na kuwalipa mishahara yao, huku wakimuomba kuendelea kuwaona zaidi.







Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.