Dk. Nandrie; Mazoezi ni kinga dhidi ya magonjwa yasiyoambukiza


FUKA-SIHA

Mkurugenzi wa Taasisi ya Tanzania Mentors Action Dk. Paul Nandrie, ameongoza maelfu ya wananchi katika mashindano ya riadha yajulikanayo kama Siha Marathon 2024, yaliyofanyika katika Viwanja vya Fuka Wilayani Siha mkoani Kilimanjaro.

Akizungumza mara baada ya kumaliza mbio za hizo Dk. Nandrie, ameisisitiza jamii umuhimu wa kufanya mazoezi mara kwa mara, kama njia bora ya kuepuka magonjwa yasiyo ya kuambukizakama vile shinikizo la juu la damu, magonjwa ya moyo, kisukari, magonjwa ya figo na kifua kikuu TB.

Amesema kuwa jamii inapaswa kujiwekea utaratibu wa kufanya mazoezi ikiwa ni pamoja na kushiriki katika mbio kama hizo ili kupunguza hatari ya kupata magonjwa hayo.

“Magonjwa yasiyo ya kuambukiza yamekuwa ni mengi sana, ili kuyatokomeza magonjwa kama haya yataondolewa kwa kufanya mazoezi ya mara kwa mara,”amesema Dk. Nandrie.

Kwa upande wake Mkurugenzi mtendaji wa halmashuri ya Siha Dk. Haji Mnasi, amesema mbio za Siha Matrathon, zimekuwa na manufaa makubwa ambapo zimekuwa zikiwa kutanisha wadau kutoka maeneo mbalimbali kuja kushiriki mbio hizo.

Aidha Dk. Mnasi, amewataka waandaaji wa mbio hizo, kujipanga zaidi kwa msimu ujao, ili wananchi na wadau mbalimbali waweze kushiriki kwa wingi katika msimu ujao.

Mwenyekiti wa halmashauri hiyo Duncan Urassa, amesema mbio hizo, zimekuwa zikisaidia kujenga afya na kuvitangaza vivutio vya utalii Wilayani humo.

“Ukosefu wa mazoezi ya mara kwa mara, huchochea magonjwa yasiyo ya kuambukiza, hivyo mbio hizi zimetusaidia sana kujenga afya zetu,”amesema Urassa.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Siha Marathon Selina Mnkony, amesema ilianza mwaka 2019, ambapo huu ni msimu wa tano tangu kuanzishwa kwake, ikiwa na malengo makubwa ya kudumisha afya za wananchi na kutokomeza ugonjwa wa kifua kikuu (TB)


















Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.