DC Mgeni; Vivutio vya Utalii Wilayani Same Vimewanufaisha Wananchi

Mkuu wa Wilaya ya Same Mkoa wa Kilimanjaro Kasilda Jeremiah Mgeni, akiwahutubia wananchi wa wilaya hiyo, wakati wa ufunguzi wa Tamasha la Same Utalii Festival Two, Desemba 20,2024. linalofanyika viwanja vya Standi kuu ya mabasi mjini humo.

SAME-KILIMANJARO.

Mkuu wa Wilaya ya Same, Kasilda Mgeni, amesema vivutio vya utalii vilivyopo wilayani humo, vimewanufaisha wakazi wa wilaya hiyo.

Hayo ameyasema Desemba 20,2024, wakati akizungumza na wananchi wa wilaya hiyo waliojitokeza kushiriki maonesho ya Tamasha la Utalii Same Festival, linalofanyika viwanja vya standi kuu ya mabasi mjini Same.

“Wageni wanapoingia Same, wanatumia usafiri, wanakula vyakulana kulala ambapo huchangia pato, lakini pia wajasiriamali wanapata fursa ya kuuza bidhaa zao,”amesema DC Mgeni.

Amesema sekta ya utalii, imeendelea kuwa nguzo muhimu katika uchumi wa mtu mmoja mmoja na kutoa fursa za ajira kwa vijana.”amesema.

Aidha amesema Serikali ya awamu ya sita,  imeendelea kufanya juhudi za kuhakikisha kwamba sekta ya utalii inapata mafanikio makubwa na kuvutia wawekezaji wengi hapa nchini, huku akitolea mfano wa filamu ya Royal Tour.”

Akizungumzia umuhimu wa Tamasha hilo Festival, mkuu huyo wa wilaya amesema, wajasiriamali wadogo wameweza kunufaika na fursa mbalimbali,  ikiwemo kuuza bidhaa zao na kujiongezea kipato na hivyo kuchangia pato la taifa.

Kwa upande wake Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Mkomazi, Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi Emmanuel Moirana, amesema uwepo wa mradi wa Mbwa mwitu na Faru ndani ya hifadhi hiyo umefanya idadi ya wageni kuongezeka kutembelea hifadhi hiyo.

Amesema kuwepo kwa  mradi wa  Mbwa mwitu na Faru idadi ya watalii, imekuwa ikiongezeka, jambo ambalo limeonyesha mwamko kwa wananchi kutembelea vivutio hivyo.

“Hifadhi ya Taifa ya Mkomazi, ilichanguliwa kama hifadhi ya uzalishaji wa Mbwa mwitu, kutokana na eneo hilo kushabihiana na mazingira  wanayoishi mbwa hao, mradi huu ulianza ukiwa na mbwa mwitu 25 ila kwa sasa wameongezeka na kufikia zaidi ya 300,”amesema.

Aidha amezitaja faida zinazotokana na Mbwa mwitu hao kuwa  ni kivutio kikubwa cha utalii hususan kwa  wageni  ambao wengi wamekuwa wakitembelea hifadhi hiyo kutokana na  uwepo  wa kivutio hicho cha mbwa mwitu.
















Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.