KALOLENI-MOSHI
Kamati ya Chama cha
Mapinduzi (CCM), Kata ya Kaloleni, imependekeza Jina la Rais Samia Suluhu
Hassani, liwe la shule mpya ya sekondari, inayojengwa katika Kata ya Kaloleni,
iliyoko halmashauri ya Manispaa ya Moshi mkoani humo.
Mapendekezo hayo yametolewa
Desemba 12,2024 na Wajumbe wa Kamati hiyo, walipokuwa kwenye ziara ya kukagua
maendeleo ya ujenzi wa miradi inayotekelezwa ndani ya kata hiyo.
Akizungumza Mjumbe wa Kamati
hiyo na Diwani wa Kata ya Kaloleni Nasibu Mariki, amesema Serikali Kuu, imeipatia
Kata hiyo kiasi cha Sh milioni 584, kwa ajili ya ujenzi wa shule mpya ya
sekondari, kutokana na kuwepo kwa msongamano mkubwa wa wanafunzi katika shule
ya Sekondari Msasani.
Mariki, amesema lengo la
kujenga shule mpya ya sekondari ndani ya kata hiyo, limetokana na changamoto
iliyowasilishwa, kwenye kikao cha Baraza la Maendeleo la Kata (WDC) kutokana na
shule ya Sekondari Msasani, kuwa na idadi kubwa ya wananchi.
Amesema shule ya sekondari
Msasani, ina takribani wanafunzi 1,400 wanaotoka kata ya Bondeni, Bomambuzi,
Mabogini na Njoro, kuja kusoma katika shule hiyo.
Aidha amesema serikali, imeleta
fedha kiasi cha Sh milioni 140, shule ya sekondari Msasani, ambazo zilitumika
kujenga vyumba vitano vya madarasa kwa Sh milioni 110, ujenzi wa maabara Sh milioni 16 na ujenzi wa matundu
saba ya vyoo kwa Sh milioni 14.
Awali akitoa taarifa ya
ujenzi wa shule hiyo Makamu mkuu wa shule ya Sekondari Msasani Godwin Momburi, kwa
Kamati hiyo amesema ujenzi wa shule mpya
ya sekondari ulianza Septemba 20 mwaka
huu na kwamba kujengwa kwa shule hiyo, itakwenda
kupunguza msongamano wa wanafunzi waliopo katika shule ya Msasani.
Akihitimisha ziara hiyo
Mwenyekiti wa Kamati ya Siasa ya (CCM), Kata ya Kaloleni Joshua Kojo, alisema kamati
imeridhishwa utekelezaji wa mradi huo, kwani thamani ya fedha inaonekana pia na
mradi huo, unatekelezwa kwa kiwango cha juu zaidi na hiyo, imeonesha ni jinsi
gani Ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) inavyotekelezwa kwa kasi zaidi.
Sambamba na hilo Mwenyekiti
huyo, amewataka mafundi wanaoendelea na ujenzi huo kuhakikisha mradi huo unakamilika
kwa wakati, ili ifikapo Januari 13, mwaka 2025 wanafunzi waweze kuingia madarasani.
Katibu wa CCM Kata ya Kaloleni
Hamadi Mgonja na Mjumbe wa Kamati ya ujenzi Happiness Urio, wameishukuru
serikali kwa namna inavyoleta fedha kwa ajili ya maendeleo ndani ya kata hiyo,
jambo ambalo, limewapunguzia mzigo
wazazi wa kuchangia fedha tofauti na huku nyuma ambapo kila mzazi litakiwa
kuchangia.
Naye Afisa mtendaji Kata ya
Kaloleni Iliyasa Mnjejah, alimshukuru Diwani Mariki kwa kujenga hoja na
kufanikisha kupata fedha za kujenga shule hiyo mpya, huku akiwaomba wananchi kuhakikisha
mradi huo wanautunza ikiwemo vifaa vinavyotumika kwenye ujenzi huo.
Mwenyekiti wa CCM Kata ya Kaloleni Joshua Odhiambo Kojo (katikati), Mjumbe wa Kamati na Diwani wa Kata ya Kaloleni Nasib Mariki wa Kwanza kushoto na Mwenyekiti wa Mtaa wa Kaloleni, ambaye pia ni Mjumbe katika Kamati hiyo Ndama wa Ndama.Moja ya Vyumba vya Madarasa shule ya Sekondari Mpya yanayojengwa kata ya Kaloleni.








