MOSHI-KILIMANJARO
Chama cha Mapinduzi (CCM) Moshi
Mjini kimesema kuwa, kura walizozipata Wenyeviti
wa Serikali za Mtaa ni ishara ya kuaminiwa na Wananchi na kuwataka Wenyeviti
hao kwenda kutatua changamoto zinazowakabili wananchi katika maeneo yao.
Faraji Swai, ameyasema hayo Novemba 28,2024 alipokuwa
akizungumza na viongozi hao kabla ya kuapishwa kwao, zoezi ambalo lililofanyika katika
ukumbi wa Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro na kuhudhiriwa na viongozi mbalimbali
wakiwemo madiwani na wananchi waliofika kushuhudia kuapishwa kwao.
Swai; amesema
wananchi wanamatarajio makubwa kwao
kuona mabadiliko halisi kupitia uongozi wao na kwamba wenyeviti hao wanahitaji kuonyesha
ufanisi katika kutekeleza majukumu yao.
Kwa upande wake Katibu wa CCM Moshi Mjini
Frida Kaaya, amewataka wenyeviti hao kutenda haki na kuonyesha uongozi
bora kwa wale wanaowaongoza.
Aidha amewataka viongozi hao kuhakikisha
kwamba wanakwenda kuzingatia haki, uwazi na uwajibikaji katika utendaji kazi
wao wa majukumu yao, ili kuleta maendeleo na kuboresha huduma kwa wananchi.
“Wenyeviti wa Serikali za Mtaa na Kamati zenu
mtakaokwenda kula kiapo chenu cha utalii muda mfupi ujao, nendeni mkayatekeleze
yote ambao chama na serikali kimewatuma, nawaombeni sana nendeni mkafanye kazi
kama timu,”amesema Kaaya.
Ameongeza kuwa “Tumemaliza uchaguzi wa serikali za mitaa jana
na leo hii tunakwenda kuanza kazi ya kuwatafutia kura za madiwani, wabunge wanaotokana na CCM pammoja na kura za Rais Samia Suluhu Hassan,”amesema Kaaya.
Akizungumza kwa niaba ya Mstahiki Meya wa
Manispaa ya Moshi Injinia Zuberi Abdallah Kidumo, Naibu Meya Stuwart Nathael, amewapongeza
viongozi wote waliochaguliwa huku akiwaomba kuzingatia kanuni za utawa bora.
Mbunge wa Jimbo la Moshi Mjini Priscus Tarimo, amesema kuwa wenyeviti hao wamebeba dhamana kubwa kwa wananchi kwenye mitaa yao na dhamana hiyo ni ya kuwatumikia wananchi.
Naye Mwenyekiti wa CCM Kata ya Soweto Paulo Maille, amesema kuwa walifanya kampeni za kistaarabu na kufanikiwa kushinda mitaa yote mitatu, huku matarajio yake ni kuona wenyeviti walioshinda wanakwenda kutimiza ahadi zao walizoziadi kwa wananchi wakati wa kampeni za uchaguzi.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti baada ya kuapishwa, baadhi ya wenyeviti akiwemo mwenyekiti wa mtaa wa kati Mussa Selemani
Kitikui, mjumbe wa serikali mtaa wa vijana Benjamin Mbisye na Musa Kitandu mtaa wa Kitandu, kwa pamoja
wameahidi kwenda kuzitimisha ahadi ambazo waliziahidi mbele ya wananchi wakati
wa kameni za uchaguzi serikali za mitaa amnbazo zilihitimishwa Novemba 26 mwaka
huu.