MOSHI-KILIMANJARO
Taasisi ya Wanawake na Wanaume wa Uchumi wa Viwanda Tanzania
Mkoa wa Kilimanjaro (WAWAUVITA) wameandaa kongamano kubwa la Wajasiriamali wadogo,
litakalofanyika Novemba 30,2024 Kata ya Uru Kusini na kuhudhuuriwa na
wajasiriamali takribani 250.
Mwenyekiti wa taasisi hiyo Mkoa wa Kilimanjaro, Mariam Mohamed Muhandeni, ameyasema hayo Novemba 29,2024 wakati
akizungumza na waandishi wa habari mjini Moshi kuelekea kongamao hilo ambapo
amesema mgeni rasmi katika kongamano hilo atakuwa Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa
wa Kilimanjaro, Shally Raymond.
Amesema lengo la kongamano hilo ni kuwakutanisha wajasiriamali
wadogo, kutengeneza vikundi vitakavyowasaidia kuweza kupata mikopo ili waweze
kujiinua kiuchumi na kuinua kipato cha mtu mmoja mmoja pamoja na taifa kwa
ujumla.
Amesema katika kongamano hilo elimu mbalimbali zitatolewa na
wataalam kutoka taasisi mbalimbali ikiwemo Benki ya Azania Bank, Shirika la
Viwango Tanzania TBS, pamoja na wataalam kutoka Shirika la Kuhudumia Viwanda
Vidogo (SIDO).
Kwa upande wake Mweka Hazina wa taaisi hiyo Magreth John amesema wajasiriamali wengi wanakabiliwa na changamoto mbalimbali zikiwemo zile za ufungashaji, upatinaji wa namba ya uborana utunzaji fedha, kupitia kongamano hilo wazalishaji hao watapata fursa kwao ya kuweza kukutana na wataalam hao wakiwemo wa TBS na kuweza kupata utaratibu wa namna ya kupata uthibitisho wa bidhaa zao.
Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Wanaume wa Uchumi wa Viwanda Tanzania Mkoa wa Kilimanjaro (WAWAUVITA) Mariam Mohamed Muhandeni.
Mweka Hazina wa Taasisi
ya Wanawake na Wanaume wa Uchumi wa Viwanda Tanzania Mkoa wa Kilimanjaro
(WAWAUVITA) Magreth Jiohn