Katibu wa NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Rabia Abdallah Hamid, akiwahutubia Wananchi na Wana-CCM Mkoa wa Kilimanjaro, wakati wa uzinduzi wa Kampeni za uchaguzi wa Serikali za Mitaa katika viwanja vya Pasua kata ya Bomambuzi Manispaa ya Moshi.
MOSHI-KILIMANJARO
Katibu wa NEC Siasa na
Uhusiano wa Kimataifa Rabia Abdallah Hamid, amewataka wanachama wa Chama cha
Mapinduzi (CCM) Mkoani Kilimanjaro, kutokudharau uchaguzi wa Serikali za Mitaa,
Vijiji na Vitongoji kwa kusema kwamba watashinda kwa kishindo.
Hayo ameyasema Novemba
20,2024, wakati wa uzinduzi wa Kampuni ya CCM ngazi ya mkoa uliofanyika viwanja
vya Pasua, Kata ya Bomambuzi , Halmashauri ya Manispaa ya Moshi mkoani humo.
Rabia ambaye pi ni mlezi wa
CCM mkoa wa Kilimanjaro, amewataka wana CCM kujitokeza kwa wingi kuwapiga kura
wagombea wa CCM ili kukiongoza chama hicho kwa kipindi cha miaka mitano ijayo.
“Uchaguzi za Serikali za Mitaa,
Vijiji na Vitongoji ni muhimu sana kuliko chaguzi zozote, kwani ndiyo msingi wa
maendeleo ya nchi, maana viongozi wa Serikali za Mitaa ndiyo waliokaribu na
wananchi hivyo ni rahisi kujua mahitaji ya kimaendeleo ili yashughulikiwe na viongozi
walioko kaytika ngazi ya chini”, alisema.
Amesema “Ushindi wa CCM
katika uchaguzi huu utakuwa ni msingi utakaokiwezesha kushinda uchaguzi mkuu
mwakaniwa Madiwani, Wabunge na Rais”, amesema.
Aidha ameendelea kusema
kuwa CCM ni chama ambacho ni tumaini kuwa kwa wananchi kutokana na uzoefu wake
wa miaka mingi tangu kupigania Uhuru wa nchi na hadi kufikia maendeleo ambayo
Taifa na wananchi wake wamepata tangu Uhuru.
“CCM imekuwa kinara kwenye chaguzi zote za serikali ya mitaa na uchaguzi mkuu kutokana na serikali zake zote kuhudumia wananchi vyema ikiwemo ile ya kuwasogozea wananchi huduma zote muhimu.”
Akiongea katika uzinduzi
huo, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kilimanjaro,Patrick Boisafi, amesema kuwa chama
hicho tawala kimesimamisha wagombea kwenye vijiji vyote 519 vilivyoko mkoani
humo.
“Nitoe kwa wito kwa wapiga
kura kujitokeza kwa wingi ili wagombea wa CCM waweze kuchaguliwa kwa lengo la
kuendelea na kazi ya kuwahudumia wananchi”, amesema Boisafi.
Amesema katika kipindi cha
miaka mitatu ya Rais Samia Suluhu Hassan, tayari serikali imeshaleta jumla ya
Sh bilioni 915 kwa ajili ya shughuli za maendeleo katika vijiji vyote mkaoni
Kilimanjaro.
Akizungumza kwa niaba ya wagombea
wa nafasi ya mwenyekiti mtaa wa Majengo Mapya kata ya Pasua Beatrice Kimambo ametoa
wito kwa wananchi kumpa ridhaa ya kuongoza mtaa huo ili aweze kushirikiana nao
katika shughuli za maendeleo katika mtaa huo.
“Katika kipindi kilichopita
nlishirikiana na wananchi wa eneo hili katika shughuli za maendeleo na matokeo
chanya yameonekana, ni matumaini yangu watanipa ridhaa tena ili kuendeleza pale
tulipoachia kupisha uchaguzi wa mwaka huu”, amesema.
Naye mgombea wa mtaa wa
Kaloleni Halmashauri ya Manispaa ya Moshi Ndama wa Ndama, amesema kuwa sera za CCM zinalenga maendeleo
na kwamba hayo yamedhihirika kwa maendeleo yaliyopatikana katika kipindi cha
miaka mitano iliyopita.