MOSHI-KILIMANJARO.
Katika kuelekea
kipindi cha miaka 63 ya Uhuru wa Tanganyika, Tanzania inatajwa kupata mafanikio
kupitia sekta ya miundombinu na huduma za kijamii.
Hayo yalibainishwa
na aliewahi kuwa mkuu wa wilaya Injinia Raymond Mushi, wakati akizungumza
katika mahojiano maalumu kuelekea miaka 63 ya Uhuru, ambapo amesema upatikanaji
wa huduma za kijamii kama afya, elimu, maji, pamoja na ujenzi wa barabara
umeimarika.
Amesema juhudi
zilizofanywa na serikali zimeleta Mapinduzi katika nyanja ya afya ikiwemo
kupunguza vifo virtokanavyo na uzazi na upatikanaji wa huduma bora za afya
katika jamii.
Aidha, amesema
mafanikio mengine yaliyopatikana katika kipindi cha kuelekea miaka 63 ya Uhuru ni
pamoja na serikali kuimarisha miundombinu ya barabara, reli, viwanja vya ndege
na bandari.
Ameongeza kuwa
serikali imeendelea pia kuimarisha miundombinu ya elimu kwa lengo la
kuhakikisha watoto wanapata elimu katika mazingira bora na yenye staha.
Kwenye sekta ya
maji Mushi, amesema huduma hiyo imeongezeka kwani kabla ya Uhuru, watu wengi
walikuwa wakitumia maji ya mifereji na mabwawa ambapo walikuwa wakichangia na
mifugo.
Aidha amesema
moja ya kazi iliyofanyika baada ya Uhuru ni kuhakikisha Tanzania inajengwa kuwa
nchi moja ya Kiswahili ambayo inatumika kuwaunganisha wananchi.
“Tanzania ni mojawapo
ya mataifa machache ya Afrika ambayo yanaunganishwa na lugha ya moja isiyo ya
kigeni, hii ndiyo lugha isiyo na kabila, dini ukanda wala kipato, ambapo watanzanaia
karibu na makundi yote wanazungunmza lugha moja ya Kiswahili.
Amesema nchi
isingekuwa na jitihada za makusudi kukifanya Kiswahili kuwa lugha ya taifa
huenda kungekuwa na matatizo mengine ambayo yanazikuta nchi nyingine.