Wanaume wenye miji mitatu, vitongoji tofauti kupiga kura kwenye eneo moja tu walilojiandikisha

MOSHI-KILIMANJARO.

Wanaume wenye miji  mitatu kwenye vitongoji tofauti, wametakiwa kuchagua kitongoji kimoja wapo watakacho kwenda kujiandikisha kwa ajili ya kupiga kura Uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika Noemba 27, mwaka huu.

Hayo yamesema Oktoba Mosi na Msimamizi wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Wilayani Mwanga, mkoani Kilimanjaro, Wakili Edwin Lusa, wakati akizungumza na Redio Kicheko Live, kuhusu maelekezo ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

Wakili Lusa amesema kujiandikisha kuwa mpiga kura zaidi ya mara moja ni kosa kisheria  na kuwataka wanaume wenye mji mitatu katika vitongoji tofauti, wanatakiwa kuchagua kituo kimoja tu kwa ajili ya kwenda kujiandikisha kupiga kura.

“Kupiga kura ni mara moja tu, wanaume wenye miji mitatua (familia zaidi ya kitongoji kimoja) wanapaswa kuchagua kitongoji kimoja wapo ambacho watakwenda kujiandikisha kwa ajili ya kushiriki uchaguzi huu.”amesema.

Amesema yako maneno ya upotoshaji yameanza kutolewa na baadhi ya vyama vya siasa, kwamba mfumo wa uandikishaji una waruhusu wanaume wenye wake watatu kujiandikisha zaidi ya mara moja, jambo ambalo amesema si kweli na ni kosa kisheria.

Katika hatua nyinginge Msimamizi wa uchaguzi huo amesema kuwa halmashauri ya Wilaya ya Mwanga inatarajia kuandikisha wapiga kura 64,000, katika uchaguzi huo.

“Kwa mujibu wa Sensa ya watu na Makazi ya mwaka 2022 watu ambao wanasifa ya kujiandikisha kwa ajili ya kushiriki uchaguzi wa Serikali za Mitaa wenye miaka wa kuanzia miaka 18 ni watu 64,000, uandikishaji huu utaanza Oktoba 11 hadi 20 mwaka huu, ambapo vituo vya uandikishaji vitafunguliwa kuanzania saa mbili kamili asubuhi hadi saa kumi mbili jioni,”amesema Wakili Lusa.

Aidha amesema vituo vya uandikishaji  katika wilaya ya Mwanga viko 291 na katika vituo hivyo wananchi watapata fursa ya kujiandikisha.








Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.