Wakazi wa Mgando waiomba Serikali kuharakisha ujenzi wa barabara ya Ndungu- Mkomazi

SAME-KILIMANJARO

Wakazi wa Kijiji cha Mgando, Kata ya Bendera Wilaya ya Same, wameiomba Serikali kuharakisha ujenzi wa barabara ya Ndungu-Mkomazi, yenye kilometa 36 inayojengwa kwa kwa kiwango cha lami.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti na Waandishi wa habari waliotembelea barabara hiyo, ili kujionea ujenzi wake wakazi hao Bony Msifuni, Michael Mbwmbo, Amir Juma na Haros Victor, wamesema kuwa kukamilika kwa barabara hiyo kwa kiwango cha lami, itakwenda kufungua fursa za kiuchumi na biashara hasa kwa  wakulima wa mpunga, ndizi na tangawizi.

Aidha wamesema kuwa  kukamilika kwa barabara hiyo kwa kiwango ncha lami vijana wengi wataweza kupata fursa za ajira kupitia shughuli za Bodaboda  hivyo kuboresha maisha yao na maendeleo ya kijiji chao.

Kwa upande wake Meneja wa Wakala Barabara (TANROADS) MKoa wa Kilimanjaro Mhandisi Motta Kyando, amesema ujenzi wa barabara hiyo ukikamilika utafungua uchumi wa wakazi wa Wilaya ya Same, ambao kwa kiasi kikubwa unategemea shughuli za kilimo cha mazao ya tangawizi, mpunga na ndizi  na kuhuisha utalii katika Hifadhi ya Taifa ya Mkoamazi.

Amesema barabara ya Ndungu hadi Mkomazi, ina kipande kilometa 36.9, amesema tayari serikali kupitia Wakala wa Barabara imesaini mkataba wa kuweza kuanza kazi ya ujenzi kwa kiwango cha lami.

Amesema mkataba wake ulisainiwa mwezi Januari mwaka huu, ambapo mradi huo utachukua miezi 18 ifikapo Desemba  mwaka 2025 kazi ya ujenzi itakuwa imekamilika.

Kyando amesema barabara hiyo endapo itakamilika itakuwa na manufaa makubwa sana, kwaniu kutakuwa na maendeleo makubwa  kwa, vijana  ambao watapata ajira na kukuza  uchumi baada ya watalii kuongezeka na watu wataona urahisi wa kufika katika hifadhi ya mkomazi.



Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.