Swai; Wananchi ni muhimu kushiriki kuwachagua viongozi wale watakaolinda maslahi ya jamii


MOSHI-MANISPAA

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Moshi Mjini na Mwenza wake Mama Mary Moshi, pamoja na familia yake wameshiriki zoezi la Uandikishaji kwenye Daftari la Wapiga kura kwa ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, katika kituo cha Zahanati Kata ya Bondeni Halmashauri ya Manispaa ya Moshi.

Akizungumza Oktoba 13,2024 mara baada ya kujiandikisha Swai amesema kuwa zoezi la kujiandikisha katika daftari la kupiga kura ni muhimu kwa kuwa ni wajibu kushiriki katika kuchagua viongozi watakaoweza kuwasaidia wananchi.

Amesema viongozi wa Serikali za Mitaa ndiyo wanaoishi jirani zaidi na wananchi hivyo ni muhimu kushiriki katika kuwachagua wale watakaolinda maslahi ya jamii husika.

Swai ameongeza kwamba upatikanaji wa viongozi wazuri unaanza kwa kujiandikisha katika mazoezi yote ya uchaguzi yanayotarajiwa hivi karibuni.

Hali kadharika Swai ametoa wito wa kipekee kwa wanawake kujitokeza katika kugombea nafasi mbalimbali za uongozi kwa kuwa wanazifahamu vema changamoto za jamii na pia wanao uwezo wa kuongoza vizuri.

Amesisitiza wananchi kushiriki vema chaguzi zote kwa amani na utulivu kwa kujiepusha na lugha zisizo na staha pamoja na vurugu wakati wa kampeni.

Nasra Faraji Swai  akijiandikisha kwenye Daftari la Wapiga kura kwa ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024.
Eva Paulo (kulia) akimsikiliza kwa makini maelekezo anayopatiwa na Mwandishi wa  Daftari la Wapiga kura Bi. Agripina Raphael kabla ya kujiandikisha katika daftari hilo.
Mary Moshakijiandikisha kwenye Daftari la Wapiga kura kwa ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024.
Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Moshi Mjini Faraji Kibaya Swai, akipata maelezo mafupi kutoka kwa Mwandishi wa Daftari la Wapiga kura Bi. Agripina Raphael kabla ya kujiandikisha.


Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.