Vituo 2,368 kutumika uandikishaji Daftari la mkazi Kiliamnajro

 Mkuu wa Mkoa wa kilimanjaro Nurdin H. Babu, akizungumza na Waandishi wa Habari kuhusu uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2024

MOSHI-KILIMANJARO.

Jumla ya vituo 2,368, vinatarajiwa kutumika kwa ajili ya wananchi mkoani Kilimanjro kujiandikishia kwenye Daftari la Mkazi linalotarajiwa kuanza Oktoaba 11, mwaka huu.

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Nurdin Babu, ameyasema hayo mnmo Oktoba 10, 2024, Wakati akizungumza na Waandishi wa habari Ofisini kwake, ambapo amesema uandikishaji wa wapiga kura utafanyika Oktoba 11 hadi Oktoba 20,2024  kwenye vituo vilivyopangwa.

Amesema wakazi wenye sifa za kupiga kura wenye umri wa kuanzia miaka 18 au zaidi na wale wanaokidhi masharti ya kisheria amewahimiza kushiriki kwa wingi katika uchaguzi huo.

“Uchaguzi wa Serikali za Mitaa ni nguzo muhimu ya Kidemokrasia ya ushirikishwaji na uwajibikaji  kwa jamii, ambapo kila mtu anahitajika kushiriki kikamilifu ili wapatikane viongozi ambao ni wawajibikaji kwa mustakabali mwema wa maendeleo ya nchi”, amesema.

Kwa mujibu wa Kanuni ya 9 ibara ya pili  ya Tanzazo la Serikali Na. 574 linalohusu Kanuni za Uchaguzi wa Mwenyekiti wa Mtaa na Wajumbe wa Kamati ya Mtaa  katika Mamlaka za Miji, maelekezo haya yanafafanua  hatua zitakazoongoza mchakato wa uchaguzi, kuanzia uandikishaji wa wapiga kura, uchukuaji na urejeshaji wa fomu  za kugombea ,uteuzi wa wagombea na tarehe ya siku ya uchaguzi.

Mkuu huyo wa Mkoa ameongeza kusema kuwa “Uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakuwa ni miongoni mwa ishara za kutekeleza misingi ya demokrasia kupitia uchaguzi huru, wazi na haki.”

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.