Kilimanjaro kuandikisha watu Ml. 1.1 uchaguzi wa Serikali za Mitaa

MOSHI-KILIMANJARO

Mkoa wa Kilimanjaro unatarajia kuandikisha watu milioni 1172,394 waliofikisha umri wa miaka 18 na kuendelea, kwa ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika Oktoba 11, mwaka huu.

Mratibu wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa mkoa Gasper Ijiko, ameyasema hayo mnamo  Oktoba 10, 2024 wakati akizungumza na waandishi wa habari Ofisini kwake kuhusu zoezi la uandikishaji wapiga kura litakalofanyika Oktoba 11 mwaka huu na kuhitimishwa Oktoba 20,2024.

Amesema maoteo ya takwimu za Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 Wanaume wanaotarajiwa kuandikishwa ni 559,676 wakati Wanawake ni 612,718.

“Mkoa wa Kilimanjaro tunatarajia kuandikisha watu ambao wamefikisha umri wa miaka 18, Wanaume wanatarajiwa kuandikishwa ni 559,676 na Wanawake ni 612, 718 ambapo maoteo yetu ya uandikishwaji ni milioni 1172,394.”amesema Ijiko.

Aidha amesema kuwa  zoezi la uandikishaji wapiga kura linatarajiwa kuanza Oktoba 11 mwaka huu hadi Oktoba 20 ambapo jumla ya vituo vya kujiandikishia katika mkoa huo viko 2,368 kuanzia vijiji na vitongoji.

Kwa upande wake Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Nurdin Babu, amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi kujiandikisha ili kuweza kutimiza wajibu wa kikatiba wa kuchagua na kuchaguliwa.

“Kama mnavyofahamu mwaka huu ni mwaka wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, ambapo tunaenda kufanya uchaguzi wa Viongozi wa Serikali za Mitaa, utakaohusisha Wenyeviti wa Vijiji, Mitaa, Vitongoji na  Wajumbe wa Serikali za Vijiji na Mitaa.”amesema.

Akizungumzia masuala la Kidemokrasia Mkuu huyo wa mkoa amesema kuwa Tanzania ni nchi Uhuru, ambapo wananchi wake wanapaswa kuamua kuhusiana na namna ya kuendesha masuala ya msingi kuhusiana na serikali zao.

Babu amesema; baada ya wananchi kujiandikisha katika daftari la Orodha ya wapiga kura, kutakuwepo na zoezi la kukagua orodha ya wapiga kura ambapo orodha yote ya wapiga kura kuanzia kitongoji hadi mtaa itabandikwa kenye mbao za matangazo, ili wananchi waliojiandikisha kutoa pingamizi katika uandikishaji wa maji yao.

“Zoezi hili litafanyika kuanzia Oktoba 21 hadi Oktoba 27 mwaka huu,”alisema Babu.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.