Msuya; Avitaka Vyama vya Siasa nchini kuteua wagombea wazuri Uchaguzi wa Serikali za Mitaa

Waziri Mkuu Mstaafu Cleopa Msuya, akijiandikisha kwenye Daftari la Wapiga kura  Serikali za Mitaa Oktoba 12, 2024 kijijini kwake Chomvu Wilaya ya Mwanga Mkoani Kilimanjaro, kulia kwake ni Mkurugenzi mtendaji halmashauri ya Mwanga Bi Zahara Msangi  na Mwandishi wa Daftari la Wapiga Kura  Kata ya Chomvu Mussa Abdallah Lupatu. 

MWANGA-KILIMANJARO

Waziri Mkuu na Makamu wa Kwanza wa Rais  mstaafu Cleopa Msuya, ametoa wito kwa Vyama vya Siasa Nchini,  kuhakikisha kwamba wanateua wagombea wenye uwezo na maadili katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika Novemba 27 mwaka huu nchini kote.

Msuya aliyasema hayo Oktoba 12,2024, muda mfupi baada ya kujiandikisha kwenye Daftari la Wapiga kura kwa ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa  mwaka huu, nyumbani kwake katika kijiji cha Chomvu  Wilayani Mwanga mkoani Kilimanjaro.

Msuya amesisitiza umuhimu wa viongozi hao kufanya kazi kwa karibu na wananchi ili kutatua changamoto zao na kuboresha maisha yao.

“Uteuzi mzuri wa wagombea utasaidia kuimarisha demokrasia na maendeleo katika maeneo mbalimbali hapa nchini.”alisema Msuya.

Aliongeza kuwa “Vyama vya Siasa nchini, ambavyo vitashiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Novemba 27 mwaka huu, wahahakikishe kwamba wanateua wagombea wazuri ambao wakibahatika kushika nafasi za uongozi watafanya kazi za wananchi kwa manufaa ya wananchi na Taifa kwa ujumla,”amesema.

“Serikali yoyote iliyoko madarakani msingi mkubwa ni Serikali za Mitaa; na hiki ni kipindi muhimu kwa wananchi kujitokeza kwa wingi na kutumia haki zao za kuchagua viongozi waadilifu ambao wataongoza Serikali za Mitaa, Vijiji na vitongoji kwa kipindi cha miaka mitano ijayo.”amesema.

Kwa upande wake Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo Zahara Msangi, amesema kuwa zaidi ya watu 84,000 wanatarajiwa kujiandikisha katika wilaya ya Mwanga, ambapo katika Kata ya Chomvu zaidi ya watu 4,000 wanatarajiwa kujiandikisha.

“Nichuku fursa hii kukushukuru wewe Waziri Mkuu Mstaafu kwa kuja kujiandikisha kwani uamuzi wako huo utaleta hamasa kubwa kwa wananchi kujitokeza kwa wingi kujiandikisha,”amesema Msangi.

Akizungumza msimamizi wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa halmashauri ya Wilaya ya Mwanga Wakili Edwin Lusa, ametoa rai kwa wananchi kutumia haki zao za msingi kwa kujitokeza kwa wingi kujiandikisha na hata kugombea nafasi zilizoko kwa mujibu wa taratibu za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Mwanga mwanahamisi Munkunda, amemshukuru Waziri Mkuu Mstaafu Cleopa Msuya, kwa kuwa mstari wa mbele na kuungana na Wananchi wa Kata anayoishi kujitokeza kuja kujiandikisha.

Munkunda alisema kila linapokuja jambo la kimaendeleo  katika ngazi ya Wilaya, ngazi ya Mkoa hata kwa ngazi ya Taifa Msuya amekuwa msitari wa mbele kushiriki jambo hilo.

Awali akiwasilisha taarifa yake Afisa mtendaji Kata ya Chomvu Omari Salim Kiangi, amesema kuwa jumla ya watu 4,291 wanatarajiwa kujiandikisha kwenye kata hiyo, ambapo alisema kati yao wanaume ni 1,822 na wanawake ni 2,469.

“Kwa siku ya kwanza lililoanza zoezi hili la uandikishaji Daftari la wapiga kura Oktoba 11, mwaka huu, mambo yalienda vizuri kwani waliandikisha jumla ya watu 991, ambapo kati yao wanaume walikuwa ni 449 na wanawake ni 522,”amesema Kiangi.Waziri Mkuu Mstaafu Cleopa Msuya, akijiandikisha kwenye Daftari la Wapiga kura Serikali za Mitaa, kushoto kwake ni Mkuu wa wilaya ya Mwanga Bi. Mwahamisi Munkunda, na kulia kwake ni Mkurugenzi halmashauri ya Mwanga Bi Zahara Msangi

Mwandishi wa Daftari la wapiga Kura Serikali za Mitaa Kata ya Chomvu Mussa Lupatu, akitoa maelezo  kwa waziri Mkuu Mstaafu Cleopa Msuya, namna zoezi la Uandikishaji wa Daftari la Wapiga kura unavyoendelea ndani ya kata hiyo.

Mkurugenzi mtendaji Halmashauri ya Mwanga Bi. Zahara Msangi, Msimamizi wa Uchaguzi Serikali za Mitaa Wakili Edwin Lusa na Diwani wa Kata ya Chomvu Shaghira Mchomvu.
Msimamizi wa Uchaguzi Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mwanga Wakili Edwin Lusa, akitoa tathmini ya namna ya Wananchi wa  Wilaya hiyo wanavyojitokeza kujiandikisha kwenye Daftari la Wapiga Kura Serikali za Mitaa
Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Mwanga Bi. Zahara Msangi, akitoa maelezo ya namna zoezi la uandikishaji kwenye Daftari la Wapiga kura Serikali za Mitaa 
 Mkuu wa Wilaya ya Mwanga Bi. Mwanahamisi Munkunda (kulia)akizungumzia suala la     Uandikishaji wa wananchi katika Daftari la Wapiga kura Serikali za Mitaa utakaofanyika Novemba 27 mwaka huu.
Waziri Mkuu Mstaafu Cleopa Msuya, Mkuu wa Wilaya ya Mwanga Bi. Mwanahamisi Munkunda na Mkurugenzi mtendaji Halmashauri ya Mwanga Bi. Zahara Msangi.
Mhe; Waziri Mkuu na Makamu wa Kwanza wa Rais Mstaafu Cleopa Msuya, Mkuu wa Wilaya ya Mwanga Bi. Mwanahamisi Munkunda na Mwandishi wa Daftari la Wapiga kura Kata ya Chomvu Bw. Mussa Lupatu.
Waziri Mkuu Mstaafu Cleopa Msuya wa tatu kutoka kulia, akiwa katika picha ya pamoja na Mkuu wa wilaya ya Mwanga Bi. Mwanahamisi Munkunda , Mkurugenzi wa halmashauri ya Mwanga Bi Zahara Msangi, Mwanasheria wa halmashauri Edwin Lusa na Diwani wa Kata ya chomvu Shaghira Mchomvu

Waziri Mkuu mstaafu Cleopa Msuya, akiwa katika picha ya pamoja na Msimamizi wa Uchaguzi Serikali za Mitaa halmashauri ya Mwanga Wakili Edwin Lusa kulia kwake na Mussa Abdallah Lupatu kushoto kwake ambaye ni Mwandishi katika Daftari la wapiga kura kata ya Chomvu.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.