Chuo cha Viwanda vya Misitu Moshi (FITI) namna kinavyotoa ajira kwa vijana

MOSHI-KILIMANJARO

Chuo cha Viwanda vya Misiti (FITI) kilichoko Moshi, mkoani Kilimanjaro kimeendelea kuboresha mitaala ya chuo hicho, lengo likiwa ni kuhakikisha mbali na kupata ajira, pia wahitimu wa chuo hicho waweze kujiajiri wenyewe.

Hayo yameelezwa Oktoba 30,2024 na Mkuu wa chuo hicho Dkt. Zakaria Lupala wakati akizungumzia mafanikio ya chuo hicho kuelekea mahafali ya 27 yanayotarajiwa kufanyika mwezi Novemba Mosi, mwaka huu.

“Chuo hiki kinatoa mafunzo ya aina mbalimali yakiwemo yale ya matumizi bora ya bidhaa za misitu na uhifadhi wa mazingira; mitaala yake pia inaboreshwa ili wanafunzi waweze kupata ujuzi utakaowawezesha kujiajiri’, alisema.

Ameendelea kusema “Mitaala yetu inalenga kuwapa wanafunzi ujuzi wa kuhifadhi raslimali za Taifa, kuwa wabunifu kupitia uchakataji wa bidhaa za misitu kwa kutumia teknolojia ya kisasa na pia kuwa wafanyabiashara wazuri wa mazao yanayotokana na misitu,” amesema.

Amesema mbali na kupata ajira, mwanafunzi anayehitimu Chuo cha Viwanda vya Misitu Moshi (FITI) anakuwa tayari amepata ujuzi wa aina mbalimbali kama vile ufundi seremala na hivyo kuweza kujiajiri yeye mwenyewe kwa kufungua karakana yake mwenyewe badala ya kusubiri kuajiriwa.

Dkt. Lupalo kusema kuwa wanafunzi wa chuo hicho hupata elimu ya ufundi kwa vitendo zaidi, ambapo alisema  kuwa pia wanapata elimu ya uzalishaji mali, ile ya upandaji na uvunaji wa miti.

Aidha amesema kuwa wanafunzi hao wanapta nafasi ya kushiriki kwa vitendo usimamizi na uhifadhi misitu, kwenye taasisi mbalimbali zikiwemo zile zilizo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii kama vile Ngorongoro, Tanapa, Tawa pamoja na taasisi binafsi.

Kwa upande wake Afisa mahusiano wa Chuo hicho Cesilia Lyimo, amesema chuo hicho kinatarajia kufanya mahafali yake ya  27 ambayo yanatarajiwa kufanyika chuoni hapo Novemba 1, mwaka huu, huku mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Katibu Mkuu (Maliasili) Wizara ya Maliasili na Utalii Dkt. Hassan Abbas.

Amesema katika mahafali hayo jumla ya wanafunzi 340 wanatarjiwa kuhitimu katika mahafali hayo baada ya kupata mafunzo chuoni hapa kwa muda wa masomo waliokuwa wamepangiwa.Mkuu wa Chuo cha Viwanda vya Misitu Moshi (FITI) Dkt. Zacharia Lupala, akizngumzia mafanikio ya chuo hicho toka kuanzishwa kwake mwaka 1976.Muonekano wa jengo la Utawala katika Chuo cha Viwanda vya Misitu Moshi FITI





Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.