
MWANGA-KILIMANJARO
Zaidi ya watu 1,360
Wilayani Mwanga Mkoani Kilimanjaro hawajui kusoma, kuandika wala kuhesabu wengi
wao wakiwa wa maeneo ya vijijini jambo ambalo linaashiria kwamba kuna haja ya
kuhamasisha elimu ya watu wazima maeneo hayo.
Hayo yamesemwa na Afisa
Elimu Watu Wazima Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga Mwl. James Tesha, wakati akisoma
risala ya kilele cha Maadhimisho ya Juma la Elimu ya Watu Wazima Ngazi ya
Wilaya, yaliyofanyika katika Chuo cha Ufundi Stadi MALAGE VTC.
Amesema kati ya watu hao wasiojua
kusoma na kuandika wanaume wako 490 na wanawake 870 na hivyo kufikisha idadi ya
watu wasio jua kusoma na kuandika 1360.
Amesema wanafunzi 14 waliokuwa
wanasoma madarasa ya memkwa walifanya mtihani na kujiunga na elimu rasmi, huku
walimu 47 waliojiendeleza kupitia elimu ya masafa waliweza kufaulu na kupata
Stashahada.
Amesema kupitia programu ya
elimu ya masafa (ODL) walimu wapatao 47 waliweza kujiendeleza kutoka ngazi ya
Astashahada kwenda Stashahada bila kuadhili kazi na wengine wanaendelea
kujiunga.
Aidha amesema halmashauri
ya Wilaya ya Mwanga ina vyuo vya ufundi vinavyomilikiwa na mashirika na watu
binafsi, ambapo vyuo hivyo hutoa fursa kwa wanafunzi waliokosa nafasi ya
kuendelea na elimu ya mfumo rasmi.
Amesema changamoto iliyojengeka
katika jamii ni kuwa na fikra kwamba elimu ya watu wazima ni kujifunza kusona
na kuandika tu na hiyo imepelekea jamii kushindwa kukitumia kitengo cha elimu
ya watu wazima.
Diwani wa Kata ya lembeni
Alexs Mwaipopo ameomba maaeneo yote ya taasisis za serikali kupimwa na kutoa
hati miliki kwa wahusika ili kuepusha mvutano na migongano ya kimasilahi ambayo
imekuwa ikijitokeza kutokana na mtu au watu kuvamia na kujimilikisha maeneo ya
serikali kinyemera.
Afisa Elimu Divisheni ya Sekondari
Wilaya ya Mwanga Reuben Mnzava, amesisitiza shule zote za sekondari wilayani
huo kuanzisha program ya ujasiriamali
kwani elimu ya ujasiriamali ni muhimu katika ngazi zote ambayo humuandaa
kijana juu ya maisha yake ya baadaye.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mwanga Zahara Msangi, ameishukuru serikali kwa kuweza kujenga vyuo vya ufundi nchi nzima, ikiwemo wilaya ya Mwanga.
Kwa mujibu wa Sensa ya Watu
na Makazi ya Mwaka 2022 Wilaya ya Mwanga ina jumla ya Wakazi 14,8763 wakiwemo
Wanawake 76,606 na Wanaume 72,157, huku watu wasiojua kusoma wala kuandika wakiwa
1,360, wanaume wakiwa 490 na wanawake 870.