Halmashauri ya Mwanga yatoa maelekezo uchaguzi Serikali za Mitaa 2024


Msimamizi wa Uchaguzi Serikali za Mitaa Wilaya ya Mwanga Wakili Edwin B. Lusa, akitoa maelezo ya uchaguzi Serikali za Mitaa, kwa wananchi walioshiriki mkutano huo ulichofanyika katika uwanja wa CD Msuya.

MWANGA-KILIMANJARO.

Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga, mkoa wa Kilimanjaro, imetoa maelekezo ya uchaguzi Serikali za Mitaa unatakaofanyika Novemba 27 mwaka huu.

Maelekezo ya uchaguzi huo, yanalenga kuwapata Wenyeviti wa Mitaa na Wajumbe Watano wa Kamati za Mitaa katika Mamlaka za Miji na Vijiji.

Akizungumza katika mkutano huo uliofanyika katika uwanja wa CD Msuya, Msimamizi wa uchaguzi wa halmashauri hiyo Wakili Edwin Lusa, amesema lengo ni kuhakikisha Taratibu zote za Uchaguzi zinafuatwa, lakini pia wagombea na wapiga kura wanapata taarifa zote zinazohitajika kwa wakati.

“Maelekezo haya yanafafanua hatua zitakazoongoza mchakato mzima wa uchaguzi, kuanzia uandikishaji wa wapiga kura, uchukuaji na urejeshaji wa fomu za kugombea, uteuzi wa wagombea na tarehe ya siku ya uchaguzi,”amesema wakili Lusa.

Aidha amesema maelekezo mengine ni yale yanayohusu  kutoa mwongozo ili kuhakikisha uchaguzi unafanyika kwa uwazi, haki na usawa na kwa kuzingatia Sheria na Taratibu zilizowekwa.

Pia Wakili Lusa amesema wanaoruhusiwa kugombea nafasi za Wenyeviti na Wajumbe  ni Watanzania wenye umri kuanzia miaka 21 na kuendelea huku wanaoruhusiwa kupiga kura ni wananchi wenye umri wa miaka 18 na kuendelea na ambao walishiriki na watakaoshiriki zoezi la uandikishaji wa wapiga kura.

“Nitoe wito kwa Wananchi wote wenye sifa, kushiriki kikamilifu katika mchakato huu wa uchaguzi, kuanzia hatua ya kujiandikisha kwenye orodha ya wapiga kura, kujiandikisha katika orodha ya wapiga kura ni hatua muhimu  inayompa kila mwananchi  mwenye sifa  haki ya Kisheria ya kushiriki  uchaguzi kama mpiga kura au mgombea.”amesema.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga Zahara Msangi, amesema kufanyika kwa uchaguzi wa Serikali za Mitaa kunawezesha wananchi kutumia haki yao ya Kikatiba ya kuomba kuongoza wenzao na kuchagua viongozi wa maeneo wanayoishi.

“Uchaguzi huu una hatua mbalimbali ambazo ni wananchi kujiandikisha kwenye daftari la orodha ya wapiga kura na mwisho kushiriki kwenye zoezi la uchaguzi.

Aidha wale wote wenye sifa za kugombea nafasi mbalimbali za uongozi kuomba nafasi hizo kupitia udhamini wa vyama vyao vya kiasiasa.

Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga Zahara A. Msangi, akitoa maelezo ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa, hafla iliyofanyika katika uwanja wa CD Msuya Wilayani humo.

Mwl. Dennis Msemo, ambaye ni mshereheshaji wa tukio la kuwahamasisha wananchi kujitokeza kwenda kujiandikisha na kupiga kura Uchaguzi Serikali za Mitaa 2024Mkuu wa Wilaya ya Mwanga Mwanahamisi Munkunda, Salehe Mkwizu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga na Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Mwanga Zahara Msangi.






 Wakuu wa Idara wakifuatilia kwa makini maelekezo ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa, yaliyokuwa yakitolewa na Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga Zahara Msangi.Mshereheshaji wa tukio la uhamasishaji wananchi kujitokeza kushiriki Uchaguzi Serikali za Mitaa Mwl. Dennis Msemo.

Afisa Uchaguzi Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga Eliamini Kishavi, (Kulia) akiteta jambo na Mshereheshaji Mwl. Dennis Msemo, wakati wa hafla fupi ya utoaji maelezo kuhusiana na Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Mwanga Mwl. Ibrahim Mnzava (Kushoto) akiteta jambo na Mwenyekiti wa UVCCM Wilayani humo.
Mwl. Abubakari H. Abdallah, mtunzi wa shairi linalohusiana na kuwahamasisha wananchi kujitokeza kwenda kujiandikisha na kupiga kura Uchaguzi Serikali za Mitaa 2024


Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.