Swai; Wafanyabiashara waliounguliwa soko la Mbuyuni kujumuishwa kwenye mpango wa kupatiwa vyumba


MOSHI-KILIMANJARO

Wafanyabiashara wote, waliounguliwa meza na bidhaa zao kwenye tukio la moto uliotokea Februari 5, mwaka 2020 na kuteketeza soko la Mbuyuni lililopo Kata ya Bondeni Halmasahuri ya Manispaa ya Moshi, watajumuishwa kwenye mpango wa kupatiwa vyumba “Flemu” kwenye mradi wa jengo jipya la soko hilo.

Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Moshi Mjini Faraji Swai, aliyasema hayo Septemba 25,2024 wakati Kamati ya Siasa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) ilipotembelea na kuangalia mradi wa ujenzi wa soko jipya la Mbuyuni, unaotekelezwa na Mkandarasi Rocktronic Ltd kwa gharama ya Sh bilioni 1.6 na kuzungumza na wafanyabiashara wa soko hilo.

Swai amesema, soko la mbuyuni ni moja ya masoko makubwa na makongwe yaliyopo katika mkoa wa Kilimanjaro, ambalo linahudumia wafanyabiashara kutoka maeneo mbalimbali.

“Februari 5, 2024 mwaka huu soko hili liliteketea kwa moto na kuacha wafanyabiashara takribani 2,500 wakiwa hawajui la kufanya baada ya bidhaa zao zote kuteketea kwa moto.”amesema.

Moto huo ambao ulioanza kuwaka majira ya saa sita usiku wa kuamkia Februari 6,2024 huku chanzo chake kikidaiwa kusababishwa na hitilafu ya umeme.

Ameongeza kusema kuwa soko hilo lina wafanyabiashara wakubwa, wadogo na wachuuzi wanaonufaika nalo kati ya Sh 20,000 hadi 50,000 kwa siku, limekuwa ni kiungo muhimu cha biashara kwa Wajasiriamali wadogo ndani ya Manispaa hiyo.









Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.