Soko la Mbuyuni kutumia Blioni 1.6

MOSHI-KILIMANJARO.

Serikali inakadiria kutumia kiasi cha Sh Bilioni 1.6 kwa ajili ya ujenzi wa soko jipya la Mbuyuni lililopo Halmashauri ya Manispaa ya Moshi mkoani Kilimanjaro.

Akitoa taarifa kwa Kamati ya Siasa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Kilimanjaro iliyotembelea na kukagua ujenzi wa soko hilo Septemba 25,2024 Mkurugenzi mtendaji Halmashuri ya Manispaa ya Moshi Mwl. Mwajuma Nasombe, amesema kwa kutambua umuhimu wa soko hilo, Baraza la Madiwani, liliitisha kikao cha dharura yakiwa ni maelekezo ya Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Nurdin Babu, kuona namna ya kutumia mapato ya ndani kwa ajili ya kuanza kujenga soko hilo.

Nasombe amesema soko hilo tayari limeanza kujengwa kwa gharama ya Sh Bilioni 1.6 ambapo halmashauri kupitia mapato yake ya ndani ilitenga Sh Milioni 800  kwa ajili ya kuanza ujenzi wa soko hilo na kati ya fedha hizo Mkandarasi ameshalipwa Sh milioni 238.

“Huko nyuma soko hilo, lilijengwa kwa tofali za udongo, kwa sasa soko linakwenda kujengwa kwa tofali za bloku na kuwekewa slabu chini, maduka 14, matundu ya vyoo 16, kupauliwa   pamoja na miundombinu ya mifereji ya maji kuzunguka soko na.”amesema

Akizungumza Meya wa Manispaa ya Moshi Mhandisi Zuberi Kidumo, amesema Baraza la Madiwani kwa pamoja, walikubaliana kusimamisha miradi mingine yote iliyokuwa inatekelezwa kwenye kata zao ili soko hilo lijengwa kwa wakati.

Naye Mbunge wa Moshi Mjini Priscus Tarimo  amesema “Soko la Mbuyuni ni eneo muhimu   kwa maendeleo ya wakazi wa Moshi mjini na viunga vyake, vikiwemo vijiji vya Shabaha, Mabogini na Mailisita vinavyotegemea huduma kwenye soko hilo.

Awalia Mwenyeki wa soko la Mbuyuni Lameck Mziray, amesema ataendelea kusimamia maelekezo ya viongozi wa chama na Serikali kuhakikishan Wafanyabiashara wote waliokuwa kwenye soko hilo kabla ya kuungua wanarudi kwenye maeneo yao.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kilimanjaro Patrick Boisafi, amewahakikishia  kila mfanyabiashara wa soko la Mbuyuni, aliyekuwa akifanya biashara katika  soko hilo atarudi bila kutoa shilingi moja.











Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.