Wakuu wa vitengo vya ununuzi watakiwa kutumia takwimu

MOSHI-KILIMANJARO.

Wakuu wa vitengo vya usimamizi wa ununuzi na ugavi, wakuu wa idara za mipango sekretarieti za mikoa na halmashauri, wametakiwa kujikita zaidi kuzitumia takwimu pindi wanapofanya manunuzi ya umma.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Kilimanjaro, Kiseo Yusuf, ametoa wito Septemba 18,2024 wakati akifungua Mkutano wa Kikanda, uliofanyika mkoani humo ukiwa na lengo la kuwakumbusha na kuwahimiza wataalam hao wanapofanya kazi zao kuzingatia Sheria ya ununuzi ya umma.

Nzowa amesema kuwa kutokana na fursa zilizopo katika Sheria ya Ununuzi wa Umma, Sheria hiyo italeta tija endapo watu wanaohusika na masuala ya ununuzi wa Umma wataifuata sheria hiyo na taratibu zote za ununuzi wa Umma.

“Matumizi ya Takwimu yana umuhimu mkubwa sana katika manunuzi ya umma, moja yanasaidia halmashauri zetu ua mikoa yetu kununua vitu kulingana na mahitaji yaliyopo, unapotaka kujenga shule katika wilaya au halmashauri flani ni lazima manunuzi yale yafanyike kulingana na mahitaji yaliyopo kwa wakati huo, pasipo kuzidisha wala kupunguza.”amesema.

Amesema kama Wataalam hawataweza kuzingatia takwimu wanaweza kufanya manunuzi ambayo wanaweza kuzidisha bila sababu ama kupunguza kwa kuwa hawana takwimu sahihi.

Amesema “Tumeona mabadiliko mazuri yaliyopo kwenye Sheria mpya ya ununuzi wa umma, ambayo kwa kiasi kikubwa yananufaisha wazawa, wito wangu kwa wanaohusika na manunuzi waifuate Sheria hii."

Kwa upande wake Meneja wa Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA) Kanda ya Kaskazini, Magai Maregesi, amewashauri Watanzania kujisajili kwenye mfumo mpya wa Kielektroniki wa Ununuzi wa Umma (NeST), ili kunufaika na Sheria hiyo inayotoa fursa za kiuchumi kwa wananchi wote wakiwamo wanawake, vijana na watu wenye ulemavu

‘’Nawasihi Watanzania kuacha kukwepa Mfumo wa NeST kwa kuwa kuna fursa nyingi kwenye Sheria ya Ununuzi ikiwemo fursa za biashara na uwekezaji, bila kujisajili wazabuni hawatatambua uwepo wao kwa wepesi’’ Amesema Maregesi.














Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.