Naibu Waziri wa Ardhi Pinda akabidhi hati miliki 250 Rombo

ROMBO-KILIMANJARO.

Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Geophrey Pinda amekabidhi  Hati Miliki za Ardhi 250 kwa wananchi wa Tarakea wilayani Rombo Mkoani Kilimanjaro.

 

Pinda amekabidhi hati hizo leo Septemba 18,2024 katika hafla fupi iliyofanyika Soko la Mbomai Wilayani Rombo Mkoani Kilimanjaro ambako Kliniki ya Ardhi ilifanyika sanjari na kupokea kero na changamoto za migogoro ya ardhi.

 

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Naibu Waziri wa Ardhi Pinda amewataka wananchi waliokabidhiwa hati kuhakikisha wanazihifadhi na kuzitunza kwa umakini pasipo kuifungasha na vitu vigumu (Lamination).

 

Aidha  amesema hati milki za ardhi walizokabidhiwa wananchi wa Rombo ni nyaraka nyeti na zina faida kubwa ikiwemo kuaminiwa kupata mikopo kutoka taasisi za kifedha nchini.

 

 

Aidha Pinda amemuelekeza Kamshina Msaidizi wa Ardhi Mkoa wa Kilimanjaro Rehema Mdee, kuendesha zoezi la kliniki ya ardhi katika wilaya hiyo kwa siku tatu kuanzia Septemba 25 hadi 27 Mwaka huu

 

Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Grophrey Pinda yuko katika ziara ya kikazi mkoni Kilimanjaro ambapo mbali na mambo mengine atasikiliza na kutatua changamoto za ardhi kwa wananchi wa mkoa wa Kilimanjaro.






 

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.