Wajane Kata ya Korongoni Wafanya dua ya kumuombea Rais Samia,

Kusanyiko la  wamama  wajane kata ya Korongoni Halmashauri ya Manispaa ya Moshi, wakiwa katika maombi maalumu ya kumuombea Raisa Samia Suluhu Hassan

KORONGONI-MOSHI

Wanawake Wajane Kata ya Korongoni Halmashauri ya Manispaa ya Moshi, wamefanya dua fupi ya kumuombea Rais Samia Suluhu Hassa pamoja na kuiombea nchi kuwa katika hali ya amani na utulivu katika kipindi cha kuelekea uchaguzi wa Serikali za Mitaa na uchaguzi mkuu mwaka 2025.

Dua hiyo ambayo ilishirikisha viongozi wa madhebu ya dini, wazee mashuhuri, viongozi wa Chama na Serikali ambayo ilifanyika katika shule ya Msingi Korongoni.

Akizungumza mara baada ya kufanyika kwa dua fupi ya kuliombea Taifa Sheikhe wa Msikiti wa Riadha Thabit Tarimo, mewataka wajane wasikate tamaa ya maisha au kujiona wanyonge pale wanapoondokewa na wenza wao;

Huku akimshukuru Diwani wa Kata hiyo kwa upendo ambao ameuonesha kwa Wajane hao kwa kuweza kuwakutanmisha kwa pamoja na kuweza kufanya dua hiyo sambamba na kula chakula nao cha mchana.

Naye mdau wa maendeleo mkoani Kilimanjaro Alhaji Ibrahim Shayo, amesema kuna mengi yanayowakumba wajane baada ya kufiwa na waume zao, kwani wengine hupambana na kufanikiwa kusonga mbele, lakini wengine hujikutana na maisha magumu wao na hata familia zao.

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Korongoni Heavenlight Kiyondo, amesema unapokuwa kiongozi mwanamke ziko changamoto nyingi ambazo anakuwa akizipitia, ikiwemo kuumizwa kwasababu tu ya kuwa kiongozi mwanamke.

Zaidi ya Wanawake Wajane 50 kutoka katika Kata ya Korongoni walishiriki dua fupi ya kumuombea Rais Samia Suluhu Hassan pamoja na kuiombea nchi kuwa katika kuelekea ucghaguzi wa Serikali za Mitaa na uchaguzi mkuu 2025.





Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.