UWT Moshi Vijijini yatoa misaada kwa watoto yatima, wazee wasijiweza

Mwenyekiti wa (UWT) Wilaya ya Moshi Vijijini Ruwaichi Kaale, akimkabidi msaada wa vitu mbalimbali kwa mzee aliyejiweza Stephano Sauli, ikiwa ni Wiki ya Maadhimisho ya Jumuiya hiyo, ambayo kimkoa  ilifanyika katika viwanja vya Zahanati ya Marry Bennett iliyoko Kata ya Kindi Wilayani humo.

MOSHI-KILIMANJARO

Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Wilaya ya Moshi Vijijini Ruwaichi Kaale, ameitaka jamii kuendelea kuwasaidia watu wenye uhitaji ndani ya jamii hata kwa mahitaji madogo, ili kutatua changamoto mbalimbali wanazokabiliana nazo.

Hayo ameyasema septemba 21,2024 wakati akitoa msaada wa vitu mbalimbali kwa watoto yatima pamoja na wazee wasiojiweza  wanaoishi Kata ya Kindi, ikiwa ni maadhimisho ya wiki ya UWT kimkoa ilifanyika katika Viwanja vya Zahanati ya Marry Bennett iliyoko Kata wilayani humo.

Kaale amewaomba Watanzania wenye uwezo kujitokeza kwa wingi kuwasaidia kwa kile walichojaliwa na Mwenyezi Mungu ili wasijione kuwa wametengwa na jamii.

“Katika maadhimisho ya Wiki ya UWT tumeweza kutoa misaada mbalimbali kwa wazee wasiojiweza na watoto yatima sambamba na kuotesha miti kwenye maeneo ya taasisi za umma,”amesema Kaale.

Mwenyekiti huyo alitumia fursa hiyo  pia kuwahamasisha wanawake wilayani humo, kujitokeza kwa wingi kuchukua fomu za kugombea nafasi mbalimbali za uongozi kwenye uchaguzi ujao wa Serikali za Mitaa ili kuchochea maendeleo hapa nchini.

“Nitoe wito kwa Wanawake wote nchini tuhakikishe tunaunga juhudi za Rais Samia Suluhu Hassan,  kwani ameleta fedha nyingi za maendeleo kwenye kila Mkoa, Wilaya na Kata,"amesema.

Amesema miaka ya nyuma mtoto alikuwa akifaulu kuwenda sekondari, mzazi alishindwa kumsomesha kutokana na kutokuwa na fedha, lakini katika kipindi cha Awamu ya Sita ya Uongozi wa Rais Samia, wazazi wanatembea kifua mbele hawadaiwi tema michango.

“Rais Samia ametoa elimu bila malipo, mtoto sasa hivi akifaulu anasoma bure ni yeye mwenyewe ashindwe.” Amesema Kaale.

Kwa upande wake Katibu wa UWT Mkoa wa Kilimanjaro Irimina Mushongi, amesema  katika  maadhimisho ya wiki UWT, walishiriki kufaya usafi nyumba ya mtumishi wilaya ya Moshi mjini, walitembelea wagonjwa hospitali ya rufaa ya mkoa wa Mawenzi, Zahanati na Vituo vya Afya, pamoja na kupanda miti zaidi ya 200 lengo likiwa ni  katika kuhifadhi mazingira.

“Tumeweza kuongeza wanachama UWT 560 na kuwasajili kwenye mfumo, pia tumeweza kuwahamasisha wananchi kujitokeza kwa wingi kushiriki uchaguzi wa Serikali za Mitaa, kujiandikishaji kwenye Daftari la Kudumu la mpiga kura na Daftari la Mkaazi, tumeweza kutoa elimu ya ukatili wa Kijinsia, lakini pia na kukutana na vikundi vya akina mama, vijana na watu wenye ulemavu na kutoa elimua ya mikopo.”amesema.Mwenyekiti wa (UWT) Mkoa wa Kilimanjaro Elizabeth Minde, akisalimiana na Mwenyekiti wa UWT Wilaya ya Moshi Vijijini Ruwaichi Kaale, baada ya kuwasili katika Kata ya Kindi. Kwenye maadhimisho ya wiki ya UWTMwenyekiti wa UWT Wilaya ya Moshi Vijijini Ruwaichi Kaale, akipanda mti, wakati wa Maadhimisho ya Wiki ya UWT Kimkoa iliyofanyika Septemba 21,2024 Kata ya Kindi Wilaya ya Moshi Vijijini.

Katibu wa UWT Mkoa wa Kilimanjaro Irimina Mushongi akisalimiana na Mwenyekiti wa UWT Wilaya ya Moshi Vijijini Ruwaichi Kaale.


Mwenyekiti wa (UWT) mkoa wa Kilimanjaro Elizabeth Minde (kushoto) akiteta jambo na Mwenyekiti wa UWT Wilaya ya Moshi Vijijini Ruwaichi KaaleMwenyekiti wa (UWT) Wilaya ya Moshi Vijijini Ruwaichi Kaale, akimkabidhi mmoja wa watoto yatima misaada mbalimbali ya kibinadamu




  Watoto yatima wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa UWT mara   baada ya kukabidhiwa misaada.

Mwenyekiti wa UWT Kata ya Kindi Pamela Mallya akisalimiana na Mwenyekiti wa UWT Moshi Vijijini Ruwaichi Kaale, mara baada ya kuwasili katika kata hiyo kwenye maadhimishi ya wiki ya UWT mkoa wa Kilimanjaro.Mwenyekiti wa (UWT) mkoani Kilimanjaro Elizabeth Minde, wa kwanza kushoto,  katikati ni Mwenyekiti wa UWT Wilaya ya Moshi Vijijini Ruwaichi Kaale na Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji UWT Mkoa wa Kilimanjaro Mwl. Lightiness Malula, wakiwa na zawadi kwa ajili ya kuwakabidhi wazee na watoto yatima.

Maria John  wa kwanza kushoto, Joseph Barnaba, Bakari Massawe na Stephano Sauli, wakiwa wamepakata zawadi mbalimbali walizokabisdhiwa na UWT mkoa wa Kilimanjaro.Wanawake wasiojiweza wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kukabidhiwa misaada mbalimbali ya kibinadamu na viongozi wa UWT, kwenye maadhimisho ya Wiki ya UWT kimkoa yaliyofanyika Kata ya Kindi Halmashauri ya Wilaya ya Moshi Vijijini.


Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.