UWT Kilimanjaro: Hatuko tayari kugawanywa kwa misingi ya vyama

KINDI- MOSHI

JUMUIYA ya Umoja wa Wanawake Tanzania wa Chama cha Mapinduzi (UWT) Mkoani Kilimanjaro umesema hauko tayari kuyumbumbishwa na kuacha ajenda yao inayolenga kumchagua Rais Samia Suluhu Hassan katika uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika nchini mwakani.

Hayo yameelezwa Septemba 21,2024 na Mwenyekiti wa UWT mkoani Kilimanjaro Elizabeth Minde, wakati wa Wiki ya Maadhimisho ya wiki ya UWT, Mkoa wa Kilimanjaro yaliyofanyikia katika Zahanati ya Marry Bennett iliyoko Kata ya Kindi, Halmashauri ya Wilaya ya Moshi, Mkoani humo.

“Sisi ajenda yetu hiyo ni kutembea na Mama ambaye ni Rais Samia Suluhu Hassani, kwa maana yakuhakikisha anachaguliwa tena kuendelea kuiongoza nchi baada ya mafanikio makubwa tuliyoyapata baada ya kushika wadhifa huo miaka mitatu iliyopita”, alisema Minde.

Minde alisema kuwa ili Umoja huo ufanikiwe kutekeleza azma hiyo ni vyema wanawake wote wakaungana na kukata hila zote zitakazowasilishwa zenye kumkwamisha Rais Samia kuendelea na kazi nzuri anazofanya.

“Tunapozungumzia ajenda ya Rais Mwanamke ni ajenda inayolenga maendeleo; tumeshuhudia katika miaka mitatu ya utawala wake Rais Samia Suluhu Hassan, amefanya kazi nyingi zikiwemo zile za kumtua Mama ndoo kichwani pampja na wanawake kuaminiwa kushika nafasi mbalimbali za uongozi na hivyo kuondoa mfumo dume uliokuwa kwenye nyanja za uongozi hapa nchini”, alisema.

Alisema kipindi kilichopita mwanamke aliachwa nyuma kwa kigezo kuwa hana elimu, lakini kwa sasa wengi wameaminiwa kushika nyadhifa mbalimbali na wamefanya na wanaendelea kufanya kazi nzuri.

“Wanawake tusiruhusu jitihada anazofanya Rais Samia kupitia utendaji wake mzuri serikalini yeye pamoja na wenzake badala yake tuunganishe nguvu zetu kwa pamoja ili kuhakikisha anaendelea kutekeleza majukumu yake kwa manufaa ya nchi”, alisema.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa (UWT) Wilaya ya Moshi Vijijini Ruwaichi Kaale, ametoa wito kwa wanawake kujitokeza kwa wingi kujiandikisha kwenye daftari la mkazi tayari kushiriki kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika mwaka huu.

“Pia nitoe rai kwa Wanawake kujitokeza wakati wa uboreshaji wa Daftari la Kudumu la mpiga kura tayari kwa ajili ya uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwakani”, alisema.

Aidha aliwataka Wanawake kujitokeza kwa wingi kuwania nafasi mbalimbali wakati wa uchaguzi wa Serikali za Mitaaa unaotarajiwa kufanyika Novemba 27 mwaka huu.

Kaale pia alitoa rai kwa  Wanawake kuhakikisha wanatangaza kazi nzuri alizofanya Rais Samia Suluhu Hassan, ikiwemo kuboresha huduma za afya, elimu, miundombinu ya barabara, umeme pamoja na sekta ya maji hapa nchini na hivyo kuwahakikishia wananchi maisha bora.

Awali akizunguimza Katibu wa UWT Mkoa wa Kilimanjaro Irimina Mushongi alisema kuwa katika kuadhimisha wiki hiyo, UWT ilifanya shughuli mbalimbali ikiwemo kufanya matendo ya huruma na kuboresha mazingira.

“Tumetembelea hospitali ya rufaa ya mkoa Mawenzi na kutoa misaada aina mbalimbali, pia tumetoa misaada kwa wazee wasiojiweza wanaishi Kata ya kindi pamoja na watoto yatima”, alisema Mushongi.

Aidha alisema pia umoja wa UWT mkoa ulishiriki katika shughuli za upandaji miti ambapo zaidi ya miti 2,000 imepandwa kwenye zahanati na vituo vya afya na maeneo mengine mbalimbali ikiwemo kwenye taasisi zinazotoa huduma za elimu.

     Wanawake wa UWT Wilaya ya Moshi Vijijini waliojitokeza kuadhimisha Wiki ya UWT Mkoa wa Kilimanjaro iliyofanyika Kata ya Kindi Halmashauri ya Moshi Vijijini.
       Wanawake wa UWT Wilaya ya Moshi Vijijini wakitabasamu
Wazee wakiwa wanafuatilia kwa makini hotuba ya Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Kilimanjaro 
Viongozi wa UWT Mkoa na Wilaya ya Moshi Vijijini wakiwapungia mikono ishara ya kuwasalimia Wanachama wa UWT Kata ya Kindi hawapo katika picha, waliojitokeza kuadhimisha Wiki ya UWT iliyofanyika Wilaya ya Moshi Vijijini.
Viongozi wa UTW Kata ya Kindi wakiwa katika Maadhimisho ya Wiki ya UWT Mkoa wa Kilimanjaro yaliyofanyika septemba 21,2024 Kata ya Kindi.
Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Kilimanjaro Elizabeth Minde, Mwenyekiti wa UWT Moshi Vijijini Ruwaichi Kaale, Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji Mkoa wa Kilimanjaro  Mwl. Lightness Malula na Katibu wa UWT Mkoa wa Kilimanjaro Irimina Mushongi,wakiwa wamebeba zawadi kwa ajili ya kuwakabidhi watoto yatima na wazee.
Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Kilimanjaro Elizabeth Minde akimkabidhi mmoja wa watoto yatima zawadi, ikiwa ni maadhimisho ya Wiki ya UWT 
Mwenyekiti wa UWT Kata ya Kindi Pamela Mallya akimkabidi mzeePaulo Leina zawadi
Katibu wa UWT Mkoa wa Kilimanjaro Irimina  Mushongi, akimkabidhi misaada ya kibinadamu Mzee Joseph Barnaba, kwenye Wiki ya Maadhimisho ya UWT Mkoa wa Kilimanjaro.
Diwani wa Viti Maalum Kata ya Kirima Aurelia Mushi, akimkabidhi sukari, mchele na mche wa sabuni ya kufulia mmoja wa wazee, ikiwa ni Maadhimisho ya Wiki ya UWT.
Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya UWT Wilaya ya Moshi Vijijini Asha Abdallah akimkabidhi mmoja wa wazee sabuni za kufulia ikiwa ni Maadhimisho ya Wiki ya UWT yaliyofanyika Septemba 21,2024 Kata ya Kindi.
     Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji Wilaya ya Moshi Vijijini, akimkabidhi mmoja wa wazee zawadi zilizotolewa na UWT katika kuadhimishi wiki ya UWT
Mwenyekiti wa CCM Kata ya kindi Juma Abdulrahman Mwisi, akimkabidhi zawadi mmoja wa wazee wakati wa Maadhimishi ya Wiki ya UWT.
Viongozi wa UWT Wilaya ya Moshi Vijijini wakimkabidhi zawadi mbalimbali mmoja wa watoto yatima ikiwa ni Maadhimisho ya Wiki ya UWT Kimkoa yaliyofanyika Wilaya ya Moshi Vijijini.
Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Kilimanjaro Elizabeth Minde, akisalimiana na akina Mama wa UWT Kata ya Kindi.
Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Kilimanjaro Elizabeth Minde (kushoto) akimlisha kipande cha keki Mwenyekiti wa UWT Moshi Vijijini Ruwaichi Kaale, wakati wa Maadhimisho ya UWT Kikoa yaliyofanyika Wilaya ya Moshi Vijijini Septemba 21,2024.
Mwenyekiti wa UWT Wilaya ya Moshi Vijijini Ruwaichi Kaale, akizungumza na Wanawake wa Jumuiya hiyo, mara baada ya kumalizika kwa maadhimisho ya Wiki ya UWT Kimkoa yaliyofanyika katika Viwanja vya Zahanati ya Marry Bennett iliyoko Kata ya Kindi Wilayani ya Moshi Vijijini.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.