Mwanasaikolojia: Vyumba vya kulala, visiwe vyumba vya mahakama

MOSHI-KILIMANJARO

Wanawake waliopo kwenye mahusiano na ndoa wametakiwa kuacha kuvigeuza vyumba vya kulala kuwa ni vyumba vya mahakama.

Hayo yamesemwa Septemba 5,2024 na Mwanasaikolojia Tiba na Ushauri Nasihi Edna Ngowi, wakati akizungumza na waandishi wa habari kwenye kongamano la Watoto Mentorship Adventure, iliyoandaliwa na Shirika lisilo kuwa la kiserikali la Inspire Change. 

Ngowi amesema  wako baadhi ya wanawake wamekifanya chumba cha kulala kuwa ni (Court Room) chumba cha mahakama, kugombana pindi mume wake anaporudi  nyumbani.

Amesema sababu ya wanaume kuchelewa kurudi nyumbani na kaumua kurejea wakati wa kula na kulala ni kwamba anajua akifika mapema nyumbani ataanza kugombezwa jambo ambalo wanaume hawpendi.

“Wanaume wengi wanarudi saa nne za usiku ni kutokana na kugombezwa hata anapokuwa chumbani amepumzia, chumba hicho kinageuka na kuwa chumba kugombana na hizo ndio sababu ambazo humfanya mwanaume kuona ni bora kupiga piga stori na marafiki zake ili akifika nyumbani ni kula na kulala tu.

“Kwenye vitabu vitakatifu vinatueleza kwamba Mwanaume ndio kichwa cha nyumba hata awe mwanaume ambaye hawezi kumudu nyumba yake, lakini bado mke unatakiwa kumheshimu kama baba mwenye nyumba, hata kama mali Mungu amekupa kuliko ya mume wako ni Mungu ameamua apitishe kwenye mkono wako wewe mke, kwani zile ni baraka za Mungu mnatakiwa mzitumie wote , kwa kuheshimiana na kupendana.

Aidha Mtaalamu huyo amesema kutokana na ugomvi pamoja na kelele za mara kwa mara ndani ya familia, zinachangia hata watoto kuwa na msongo wa mawazo na kutoa wito kwa wana ndoa hao ni muhimu kuzungumza kwa upendo ili kutatua matatizo hao ili kuweza kujenga uhusiano wenye afya njema.

Kwa upande wake mkufunzi na mboreshaji wa afya ya Jamii Dkt. Sabina Mtweve, amesema changamoto inayo waathiri watoto wengi kiafya kwa sasa ni kutumia muda mwingi ni kucheza gemu pamoja na kuangalia picha chafu mitandaoni, jambo ambalo linasababisha hata uwezo wao wa kudadisi unapungua kutokana na kupata taarifa mbalimbali kuingia kwenye akili zao.




 

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.