Kampuni ya Pamoja Occasion Organisers Limited yazindua kinywaji baridi kinavyotokana na zao la Kahawa

MOSHI-KILIMANJARO

Kampuni ya Pamoja Occasion Organisers Limited ya Mjini Moshi Mkoani Kilimanjaro, imezindua vinywaji baridi vinavyotokana na zao la Kahawa.

Uzinduzi wa kinywaji hicho  ulifanyika Septemba 9,2024, ambapo ulioenda sambamba na uzinduzi wa Tamasha la tano la msimu wa Kahawa (Kahawa Festval-2024) uliofanyika katika ukumbi wa mnada wa Bodi ya Kahawa Tanzania TCB.

Akizungumza katika hafla hiyo ya uzinduzi Mkurugenzi wa Kampuni ya Pamoja Occasion Organisers Limited Vicent Mulungwana, amesema utengenezajia wa kinywaji cha kahawa baridi, umeongeza mahitaji ya watu kukitumia kinywaji hicho huku akisema kuwa, wengi ambao walikuwa wanakataa kukitumia kinywaji hicho kwa sasa wamekuwa kimbilio la  bidha hiyo kutokana na ladha yake  kuwa nzuri.

"Kinywaji hiki kinatumiwa na watu wote kuanzia mtoto mdogo hadi watu wazima, watu wanapo tumia kinywaji hiki ambazo mtumiaji anaweza kuzipata ikiwemo  kukabiliana na maradhi mbalimbali kama vile saratani, maradhi ya moyo, kiharusi pamoja na kuondoa magonjwa ya uzee na hivyo  kumfanya mtu huyo aweze kuishi maisha marefu."amesema.

Anazitaja zaida zingine zitokanazo na unywaji wa kahawa huo kuwa, mbali na kupoteza kumbukumbu pia hulinda afya ya ini, huondoa msongo wa mawazo, na hukabiliana na maradhi mbalimbali.

Amesema tu yeyote anayetumia kahawa hiyo baridi kwanza inamsaidia kwenye mwili wake kupata mzunguko wa damu kukaa vizuri pia ina muwezesha kupata joto la mwili na joto la damu kukaa sawa,

Vilevile  ina msaidia kutokuugua vidonda vya tumbo, kurejesha kumbukumbu kwenye kongosho lakini pia inakwenda kusafisha mafuta ambayo yanakuwa yamejikusanya juu ya utumbo na hivyo kumsaidia kula chakula vizuri na kunywa maji kwa wingi hivyo kuufanya mzunguko wake wa damu kuwa sawa.

Katika hatua nyingine Mlungwana ameipongeza Bodi ya Kahawa Tanzania (TCB) kwa kuendelea kuwahamasisha Watanzania kuongeza hamasa ya unywaji wa kahawa ili kuboresha afya zao sambamba na kuimarisha soko la ndani la zao hilo.

“Kutokana na TCB kuendelea, kuwahamasisha Watanzania kunywa kahawa ya ndani kwa sasa kuna mabadiliko makubwa ya wananchi kutumia bidhaa za ndani zinazotokana na zao la kahawa.”amesema,

Akizindua msimu wa tano wa Tamasha la Khawa (Kahawa Festival-2024) Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Nurdin, ameipongeza Kampuni ya Pamoja Occasion Organisers Limited kwa kutengeneza kinywaji hicho ambacho kitakwenda kuongeza unywaji wa kahawa wa ndani.

“Kahawa ni zao la kiuchumi na tegemezi kwa Mkoa wa Kilimanjaro na nchi kwa ujumla, hivyo utamaduni na desturi ya unywaji wa kahawa utaimarisha sana soko letu la ndani na kupunguza utegemezi kwenye soko la kimataifa kwani bei inapoyumba katika soko la dunia huathiri moja kwa moja pato na uchumi wa mkulima na Serikali kwa ujumla.”amesema Babu.






 

 

 

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.