Halmashauri Kuu ya CCM Wilaya ya Moshi Vijijini yaipongeza RUWASA

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Moshi Vijijini Cyrili Mushi, akijadili jambo na Katibu wa CCM Moshi Vijijini Ramadhan Mahanyu. 

MOSHI-KILIMANJARO

HALMASHAURI Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Moshi Vijijini, Mkoani Kilimanjaro, imeupongeza uongozi wa Wakala ya Usambazaji Maji na Usafi na Mazingira Vijijini (RUWASA) kwa kutekeleza miradi ya maji ambayo imeweza kutatua changamoto za uhaba wa maji ambao ulikuwa ukiwakabili wananchi wengi wilayani humo.

Mwenyekiti wa CCM Moshi Vijijini Cyril Mushi alitoa pongezi hizo Septemba 13,2024 wakati kikao cha halmashauri hiyo kilichofanyika Ukumbi wa mikutano wa Ofisi za CCM  mkoani humo.

Amesema moja ya changamoto kubwa ambazo huwakabili wananchi ni ile ya upatikanaji wa Maji Safi na Salama; huku akiwapongeza RUWASA Moshi Vijijini kazi kubwa ya kukabiliana na changamoto hiyo kwa kutekeleza miradi mingi ya maji.

Akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2020-2025 kwenye kikao hicho kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Moshi James Kaji, Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Moshi David Mgonja, amesema moja wapo ya kazi kubwa iliyofanywa ni kuboresha na kuimarisha miundombinu ya maji.

Amesema moja ya kazi zilizofanyika ni pamoja na ukukarabati mradi ya maji Marangu katika kata za Marangu  Magharibi na Marangu Mashariki ambapo mradi huo unahudumia vijiji 11, na kwamba utekelezaji wake umefikia asilimia 70.

Amesema katika kutekeleza miradi hiyo ya maji, wananchi katika vijiji 9 vya kata za Kibosho Kirima, Kibosho Kati, Okaoni na Kirua Vunjo watanufaika na utekelezaji wa miradi ambayo inaendelea kufanyika huko.

Akizungumzia ukusanyajin wa mapato Afisa Mipango huyo amesema Halmashauri hiyo imeendelea kuimarisha ukusanyaji wa mapato kwa kuboresha mifumo ya ukusanyaji wa mapato hayo.

Vilevile amesema katika kipindi cha miaka minne kuanzia mwaka 2020/2021 na 2023/2024 ukusanyaji wa mapato umeongezeka kutoka Sh bilioni 2.9 na kufikia Sh bilioni 4.1 mwaka 2023/2024.

Aidha amesema kuwa Halmashauri hiyo pia imeendelea kubuni vyanzo vipya vya mapato ikiwemo kuanzishwaji wa Standi mpya ya daladala  eneo la Sango.

Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Moshi Vijijini Cyrili Mushi, akisisitiza jambo wakati akiendesha kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM Wilaya ya Moshi Vijijini.

Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Moshi Vijijini Shadrack Mhagama (Kulia) akijadiliana jambo na Katibu wa CCM Wialaya ya Moshi Vijijini Ramadhan Mahanyu.

Mjumbe wa Baraza KUU (UVCCM)Taifa Victor Makundi, akisalimia na Katibu wa CCM Wilaya ya Moshi Vijijini Ramadhan Mahanyu, baada ya kumalizika kwa kikao cha Halmashauri KUU ya CCM Wilaya ya Moshi.

Mwenyekiti wa UVCCM Kata ya Makuyuni Sunday Abdul Chilembwe wa kwanza kushoto, Mjumbe wa Baraza Kuu la UVCCM Taifa Victor Makundi katikati na Emmanuel Mlaki wa kwanza kulia wakibadilishana mawazo mara baada ya kumalizika kwa kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM Wilaya ya Moshi Vijiji nje ya Ofisi za CCM Mkoa wa Kilimanjaro

Mjumbe wa Baraza KUU (UVCCM)Taifa Victor Makundi, alisalimia na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi CCM Wilaya ya Moshi Emmanuel Mlaki.

Wakili Msoni Emmanuel Mlaki (Kulia) akiteta jambo na Mjumbe wa Baraza KUU (UVCCM)Taifa Victor Makundi.

Mwenyekiti wa CCM Moshi Vijijini Cyrili Mushi akimnong'oneza jambo Katibu wa CCM Wilayani humo Ramadhan Mahanyu.

Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Moshi Vijijini wakifuatilia uwasilishwaji wa taarifa ya Ilani ya Uchaguzi ya mwaka 2020-2025 iliyowasilishwa  SEptemba 13,2024 na Mkuu wa Wilaya ya Moshi James Kaji.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.