PICHA: Zuberi Cup Tournament 2024: Msaranga yatinga robo fainali ikiizabua Badland 2-0

 

Katibu wa Kamati ya Mashindano ya Zuberi Cup 2024 Pascal Mhere.

● Ukiwa ni msimu wa nne toka kuanzishwa kwa mashindano hayo mwaka 2020.

● Tumeanza hatua ya 16 bora , timu takribani 16 ambazo zimepata nafasi ya kufika hatu ya hiyo kati ya zile timu 44.

● Timu hizo zimeanza Julai 20, 2024 kwa mchezo ambao umezikutanisha timu ya Msaranga FC na Timu ya Badland FC ambazo zimefungua dimba la kucheza , na kumalizika kwa Msaranga kuibuka na ushindi wa 2-0 lakini pia kutakuwa na michezo mingine hadi Julai 27 mwaka huu.

● Tangu kuanza kwa mashindano hayo tumeshuhudia ushindani mkubwa umezidi kuonekana kati ya timu moja hadi nyingine.

● Tuna washukuru wadau mbalimbali ambao wameendelea kuona thamani ya mashindano hayo wakiwemo AZANIA BANK ambao wameona kunanhaja ya kuongeza nguvu katika maahindano hayo.

● Wamejitolea kutoa zawadi ya mchezaji bora kila mchezo utakaokuwa ukichezwa, pia watatoa zawadi kwa golikipa , mshambuliaji bora, mchezaji bora wa mashindano na watatoa pia na zawadi kwa kikundi cha uhamasishaji.






Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.