MOSHI, STENDI KUU-KILIMANJARO
Wajasiriamali wa vyakula maarufu Mama Lishe katika
Stendi Kuu ya Mabasi mjini Moshi mkoani Kilimanjaro wamepeleka kilio
chao kwa Manispaa ya Moshi kuhusu changamoto mbalimbali zinazowakabili
wakitaka majibu yenye kuridhisha ikiwamo kiwango cha ushuru wanachotozwa
kwa mwezi.
Mama
Lishe hao wapatao 150 kati ya wafanyabiashara 467 waliosajiliwa katika
stendi hiyo wamekuwa na changamoto lukuki ambazo zimekuwa zikiwakwamisha
kutatua changamoto za kifamilia ikiwamo kujipatia malazi, mavazi na
chakula kwa ustawi bora.
Wakizungumza
na Diwani wa Kata ya Mawenzi Apaikunda Naburi aliyefika katika stendi
hiyo na kufanya mkutano wa hadhara wa kujua kero zao ili zipewe utatuzi
wa haraka kwa maendeleo yao na taifa kwa ujumla
Aidha
Mama Lishe hao wametaka hatua za haraka zichukuliwe dhidi ya watoa
huduma wenzao wa vyakula ambao huingia stendi hapo kwa kificho hivyo
kukwepa ushuru ambapo wachache ndio wanaobeba mzigo huo.
Katika
suala la mama lishe wanaokwepa ushuru, Mwenyekiti wa Akina Mama Lishe
Manispaa ya Moshi Florah Meena, amesema wako baadhi ya akina lishe
wamekuwa wakija alfajiri na kuzaa vyakula kwenye maeneo hayo na
inapofika majira ya saa moja asubuhi huondoka pasipo kulipa ushuru.
Aidha
katika changamoto ya miundombinu ya maji inayowawezesha kumwaga maji
katika stendi hiyo, Salma Richard, amesema eneo walilotengewa kufanyia
biashara ya chakula hakuna sehemu ya kumwaga maji machafu pindi
wanapoosha vyombo na wanapo kutwa wakimwaga maji hayo chini hutozwa
faini ya Sh elfu 10 na uongozi wa standi hiyo.
Meneja
wa Standi Kuu ya Mabasi Moshi Hashimu Kilongola, amesema wako kwa akina
mama lishe wamekuwa wakitokea maeneo ya Bomang'ombe, KCMC, Rau,
Machame, Njoro, na Shirimatunda na kuondoka asubuhi na hivyo wamekuwa
na wakati mgumu wa kuwadhibiti.
Diwani
wa Kata ya Mawenzi Apaikunda Nabur, amesema kikao hicho
kiikuwakimelenga kukutana namakundi ya watu wa chini ambao wanafanya
biashaara ndani ya standi kuu ya mabasi na akusikiiza kero zao kwani
makundi hayo ndiyo yenye changamoto nyingi.
Kwa
upande wake Mwenyekiti wa CCM Kata ya Mawenzi Mujibu Abeid, alitumia
fursa hiyo kumuagiza Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya
Moshi Mwajuma Nasombe, aliyewakiishwa na Meneja wa Stendi hiyo,
kuhakikisha kwamba mama lishe wote wanaofanya biashara ndani ya standi
hiyo wanalipa ushuru.