Balozi Mtumbuida atoa wito kwa Diaspora uchaguzi mkuu Msumbiji Oktoba 9, 2024

 

Balozi wa Msumbiji nchini Tanzania (mwenye suti ya kijivu) Ricardo Mtumbuida akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Kamati ya Siasa ya Mkoa wa Kilimanjaro mnamo Aprili 17, 2024 alipozuru mkoani hapo kwa ajili ya kutoa wito kwa Diaspora kuhusu uchaguzi wa taifa la Msumbiji utakaofanyika Oktoba 9, 2024. (Picha na KISENA)

MOSHI,CCM-MKOA KILIMANJARO

Balozi wa Msumbiji nchini Tanzania Rocardo Amrosio Mtumbuida amewataka raia wa taifa hilo wanaoishi nchini Tanzania kujiandaa kupiga kura katika uchaguzi mkuu wa taifa hilo utakaofanyika baadaye mwaka huu.

Akizungumza mjini Moshi, mkoani Kilimanjaro kaskazini mwa Tanzania waati wa ziara yake ya siku moja Balozi huyo aliuambia mkutano wa viongozi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) chenye mafungamano na chama cha FRELIMO nchini Msumbiji kuwa raia wa Msumbiji wanaoishi nje ya taifa lao kuwa mwaka huu ni mwaka wa uchaguzi.

“Watu wa Msumbiji mwaka huu tunaelekea kwenye Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Wakuu wa Mikoa, Tayari uchaguzi wa Serikali za Mitaa ulishafanyika mwaka jana, sasa tunaelekea kwenye uchaguzi mkuu mwaka huu,” alisema Balozi Mtumbuida.

““Nimekuja kuwaomba viongozi wangu wa CCM mtusaidie kuwahamasisha raia wetu wa Msumbiji wanaoishi Kilimanjaro, itakapofika Oktoba mwaka huu wajitokeze kwa wingi kwanda kukipiga kura chama cha Frelimo ili kiweze kuendelea kuwa imara,” alisisitiza.

Balozi Mtumbuida amesema miaka mitano iliyopita kumefanyika mabadiliko mengi katika katiba yao likiwamo suala la uchaguzi wa wakuu wa mikoa ambalo hapo awali halikuwepo ambapo mwaka huu watafanya uchaguzi wa viongozi hao

“Bunge wa Msumbiji lina viti 250 na chama cha Flelimo kinaongoza kwa asilimia 94 ya Wabunge wote, na uchaguzi wa mwaka huu tunatamani kufikia asilimia 100. Kipindi cha miaka mitano iliyopita zoezi la kuwachagua Wakuu wa Mikoa  halikuwepo , lakini baada ya mabadiliko ya Katiba kwa mara ya kwanza tunakwenda kufanya uchaguzi wa Wakuu wa Mikoa,” aliongeza Balozi Mtumbuida.

Oktoba 9, 2024 Msumbiji itafanya uchaguzi mkuu, ambapo Diaspora wa Msumbiji waliopo nchini Tanzania hususani mkoani Kilimanjaro watakuwa na kituo cha wapiga kura siku hiyo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Moshi Mjini Faraji Kibaya Swai; alisema ziara ya Balozi wa  Msumbiji nchini Tanzania  imemkumbusha mambo mengi sana, wakati ule wa harakati za kutafuta ukombozi  Kusini mwa Afrika, Tanzania ilikuwa mstari wa mbele chini ya Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere,  ambaye aliweza kuweka undugu baina yetu na Msumbiji.

“Nakumbuka nikiwa Chuoni , tulikuwa tunatoa damu kwa ajili ya wapigania Uhuru kule nchini Msumbiji , undugu wetu na nchi ya Msumbiji ni damu.Ninamshukuru sana Balozi ameonesha kuendeleza undugu wetu  kwa kuja katika mkoa wetu wa Kilimanjaro hususan hapa Moshi mjini na kuzungumza na Wanachama wa CCM,” alisema Swai.






 

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.