Waliofariki kwa Mafuriko Moshi Vijijini waagwa

 

Watu watano waliofariki kwa mafuriko wilaya ya Moshi mkoani Kilimanjaro wameagwa leo asubuhi katika viwanja vya Halmashauri ya Wilaya hiyo na mamia ya waombolezaji.

Tito Chaki (1961-2024), Joram Kimambo (2011-2024), Freddy Justus (2018-2024), Anjela Chaki (2012-2024) na Edward Chaki (2010-2024) wa familia moja waliopoteza maisha katika janga hilo.

Walikutwa na umauti mnamo Aprili 25 mwaka huu, kutokana na Mvua kubwa zinazoendelea kunyesha nchini ambazo zimeleta athari kubwa ikiwamo vifo, uharibifu wa mashamba, nyumba, madaraja na barabara.

Viongozi wa Siasa na dini wamehudhuria Ibada hiyo na marehemu hao wanatarajiwa kuzikwa katika kata Mbokomu na Kimochi. wilayani humo.

Bwana Ametoa, Bwana Ametwaa; Jina lake Lihimidiwe.....AMEN


 

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.