MWIKA-KUSINI.
Mgombea Udiwani wa
Kata ya Mwika Kusini, kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), John Robert Tarimo, Agosti
2, 2025, amewasilisha vipaumbele vyake vitano kwa Wajumbe wa chama hicho, katika
mkutano wa chama hicho uliofanyika eneo la Ghorofani, kijiji cha kondeni,
kitongoji cha kisharrini.
Katika hotuba yake, Tarimo aliahidi kushughulikia
changamoto sugu zinazowakabili wakazi wa kata hiyo endapo atapewa ridhaa ya kupeperusha
bendera ya CCM katika Uchaguzi wa Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani
utakaofanyika Oktoba 29 mwaka huu.
Alisema “Kipaumbele chake
cha Kwanza; Ni kuhakikisha Kata ya Mwika Kusini inapata kituo cha afya,” alisema Tarimo na kuongeza kuwa kwa miaka mingi kata
hiyo imekuwa bila huduma ya afya ya uhakika, kinyume na matakwa ya Ilani ya CCM
inayotaka kila kata kuwa na kituo cha afya, ameahidi kushirikiana na Serikali
pamoja na chama kuhakikisha kituo hicho kinapatikana.
Kipaumbele cha Pili Maji, Tarimo alisema tayari
ameanza kufanya utafiti wa vyanzo vya maji vilivyopo ndani ya ardhi ya Mwika
Kusini. “Tayari nimebaini vyanzo vya
maji, na endapo nitachaguliwa, nitashirikiana na Mamlaka husika pamoja na wadau
mbalimbali kuhakikisha tunapata chanzo chetu cha maji na kujenga tanki kubwa
litakalotatua tatizo la maji kabisa,” alieleza.
Katika
kipaumbele cha Tatu, Tarimo aligusia
usalama wa wakazi kwa kuahidi kusimamia upatikanaji wa kituo cha polisi katika
kata hiyo kwa kushirikiana na Serikali na wadau wengine.
“Barabara
ni kichocheo cha maendeleo, watu wanashindwa kusafirisha mazao yao kwa sababu
ya barabara duni, nataka kuandika historia katika suala hili,” alisema.
Kipaumbele
cha Tano; ni ujenzi wa ofisi ya Serikali
ya Kata. Tarimo aliahidi kushirikiana na watu wenye asili ya kata hiyo
wanaoishi nje ili kusaidia kujenga ofisi hiyo kwa ajili ya kuboresha utoaji wa
huduma kwa wananchi.
Mkutano huo ulihudhuriwa na Wajumbe mbalimbali wa CCM kutoka maeneo tofauti ya kata hiyo, na ulifanyika kwa utulivu huku Wajumbe wakisikiliza kwa makini na kuonyesha matumaini juu ya ahadi hizo.
.jpg)





