NASOMBE; AFICHUA MAFANIKIO KUONGEZA KWA MAPATO YA HAMASHAURI YA MANISPAA YA MOSHI, KUTOKA ASILIMIA 32 HADI 75 KATIKA KIPINDI CHA MIAKA MINNE YA RAIS SAMIA


MOSHI-KILIMANJARO.

Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi Mwl. Mwajuma Nasombe, amesema kuwa kwa kipindi cha miaka minne ya uongozi wa serikali ya awamu ya sita Manispaa hiyo imekuwa kimapato kutoka asilimia 32 hadi kufikia asilimia 75.

Akizungumza na Waandishi wa habari ofisini kwake jana Mwl. Nasombe amesema kuwa kuongezeka kwa mapato hayo kumechangiwa na miundombinu sahihi ya ukusanyaji wa mapato,

Mwl. Nasombe amesema kuwa katika upande wa ushuru wa masoko makadirio kwa mwaka ni kukusdanya kiasi cha Sh milioni 298 ambapo mpaka sasa tayari wamekusanya Sh milioni 220 jambo ambalo linaonesha kuwa huwenda wakavuka makadirio hayo.

Aidha amesema kuwa Manispaa hiyo iliamua kukusanya mapato yenyewe baada ya kuona kuwa mawakala walikuwa wameshuka kiwango kilichokuwa kimekusudiwa.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.