TRA Kilimanjaro yatoa msaada wa magodoro 50 Gereza Kuu Karanga

MOSHI.

Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA Mkoa wa Kilimanjaro wametoa msaada wa mahitaji muhimu kwa wafungwa na mahabusu wanaotumikia kifungo katika Gereza la Karanga ikiwa sehemu ya kurejesha kwa jamii katika kuelekea siku ya wiki ya Shukrani kwa Mlipa kodi.

Akizungumza wakati wa kukabidhi msaada huo Meneja wa TRA Mkoani hapa James Jilala wamesema wameona ni vema kuwashika mkono wafungwa hao ambao wana uhitaji mkubwa.

“Tunafahamu kwamba serikali inafanya jitihada kubwa katika kuwahudumia wafungwa na mahabusu walioko magerezani, lakini na sisi TRA tumeona tuje kuwashika mkono wenzetu hawa walioko hapa gerezani ikiwa ni sehemu ya shukrani kwa mlipa kodi.”alisema.

“Mamlaka ya mapato Tanzania, tuliona ni muhimu kujumuika na wenzetu hawa, ambapo leo  tumekuja kuwakabidhi magodoro 50 gereza kuu la Karanga,”alisema Jilala.

Akipokea msaada wa magodoro 50 yaliyotolewa na TRA mkoani hapa, Mkuu wa Magereza Mkoa wa Kilimanjaro,Kamishna Msaidizi wa Magereza SACP Leornad Burushi,alisema mahitaji ni makubwa na kwamba bajeti ya serikali haitosherezi mahitaji ya gereza hilo lenye wafungwa wengi.

“Magodoro ambayo yamekuwa yakinunuliwa na serikali hayatosherezi mahitaji ya wafungwa na mahabusu walioko katika gereza hilo, tunawashukuru sana TRA kwa kutuletea magodoro haya hapa gereza kuu Karanga,”alisema.

Alisema kuwa TRA sio mara yao ya kwanza kuleta misaada hapa, wamekuwa wakitukumbuka katika nyakati tofauti na kwa msaada huu kwetu unakwenda kupunguza changamoto iliyop,” alisema.






Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.