Utunzaji bora wa kumbuklumbu, msingi wa mafanikio ya biashara

Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Kilimanjaro Shally Raymond, akizungumza kwenye kongamano la  Wanawake na Wanaume wa Uchumi wa Viwanda  Tanzania Mkoa wa Kilimanjaro (WAWAUVITA) lililofanyika Kimanganuni, Kata ya Uru Kusini , Halmashauri ya Moshi Vijijini mkoani Kilimanjaro kuhudhuuriwa na Wajasiriamali takribani 250.

MOSHI-KILIMANJARO

Imeelezwa kuwa utunzaji bora wa kumbukumbu husaidia wajasiriamali kufuatilia maendeleo ya biashara zao, kutathmini faida na hasara na kutoa mwelekeo sahihi katika kupanga mikakati ya ukuaji wa biashara zao.

Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Wanaume wa Uchumi wa Viwanda Tanzania Mkoa wa Kilimanjaro (WAWAUVITA), Mariam Muhandeni, aliyasema hayo jana wakati akizungumza katika kongamano la (WAWAUVITA) lililofanyika Kimanganuni, Kata ya Uru Kusini na halmashauri ya Moshi vijijini mkoani Kilimanjaro kuhudhuuriwa na wajasiriamali takribani 250.

Amesema utunzaji mzuri wa kumbukumbu za biashara , husaidia kujua muda unaopaswa kuagiza bidhaa husika huku akisema kuwa ni makosa katika biashara kuishiwa bidhaa inayohitajiwa na wateja kwani mjasiriamali anaweza kupoteza wateja wake.

Aidha amesema kuwa sio vizuri  kuwa na akiba ya bidhaa nyingi ambayo hainunuliki, huku akisistiza pia ni muhimu  mjasiriamali kujua hali ya kifedha ya biashara yake, wakati wowote ili kuepuka changamoto zinazoweza kutokea.

Naye Katibu wa Wawauvita Joseph France Aloyce, amesema wajasiriamali wengi wanashindwa kufanikiwa na kupiga hatua kutokana na kukosa umakini katika kutunza kumbukumbu za biashara.

“Kadri biashara yako inavyokua na idadi ya shughuli za kibiashara zinavyoongezeka, inakuwa vigumu kufuatilia manunuzi, mauzo, mali, fedha taslimu, wadai na wadaiwa, hivyo kuna umuhimu wa kuwa na kumbukumbu za biashara,”amesema Aloyce.

Akifundisha katika semina hiyo Meneja wa Benki ya Azania tawi la Moshi Yusuf Lenga, amewataka wakazi hao wa Uru Kusini kuachana na utaratibu wa kujiunga katika vikundi kwa nia ya kutaka fedha.

Wengine waliopata fursa ya kufundisha ni Mhadhiri kutoka Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi (MoCU) Beatrice Kimaro ambaye amewataka wajasiriamali hao kujitahidi kuwa na matumizi mazuri

Awali akizungumza katika kongamano hilo Diwani wa Kata ya Uru Kusini halmashauri ya Wilaya ya Moshi Vijijini mkoani Kilimanjaro, Wilhard Kitali, amewataka wakulima wa ndizi kuungana kwa pamoja katika utaratibu unaofaa ili kuhakikisha soko la zao hilo halichezewi na wachache wanaotaka kujinufaisha kupitia wakulima hayo.

“Hali iliyopo kwa sasa kwa wakulima wa ndizi wa Uru Kusini Mkungu mmoja wa ndizi umekuwa ukinunuliwa shambani kwa shilingi 3,000 hadi shilingi 5,000, kisha unauzwa kwa zaidi ya shilingi 15,000 kwenye masoko makubwa nchini baada ya walanguzi kuchukua shambani hatua ambayo imekuwa mwiba kwa wakulima.”amesema.

Mweka Hazina wa taasisi hiyo  Magreth John amesema wajasiriamali wengi wanakabiliwa na changamoto mbalimbali zikiwemo zile za ufungashaji, upatinaji wa namba ya ubora na  utunzaji fedha, kupitia kongamano hilo wazalishaji waliweza kupata fursa kukutana na wataalam mbalimbali wakiwemo wa TBS  na kuweza kupata utaratibu wa namna ya kupata uthibitisho wa bidhaa zao.

Kwa upande wake Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Kilimanjaro Shally Raymond, alipata fursa ya kuzungumza na wajasiriamali hao wa Uru Kusini na kuongeza kuwa wakulima wenye elimu ya fedha wanaweza kuelewa na kuchagua mikopo bora kutoka kwa taasisi za kifedha kama vile benki na vikundi vya kifedha na kwamba kupitia mikopo hiyo, inaweza kutumika kupanua shughuli za kilimo.

“Wakati watu wanapokuwa na elimu ya fedha, wanakuwa na tabia bora za kifedha kama vile kuwekeza, kulipa kodi, na kuchangia katika uchumi wa taifa, hii inaongeza ustawi wa jamii na taifa kwa ujumla.













Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.