MWANGA-KILIMANJARO
Serikali Wilayani Mwanga, mkoani
Kilimanjaro imeipongeza Kampuni ya Kisangara
Tours Ltd, kwa kutoa mchango mkubwa katika kuvitangaza vivutio vya utalii vilivyomo
wilayani humo.
Pongezi hizo zimetolewa hivi
karibuni na Mkuu wa Wilaya hiyo Mwanahamisi Munkunda, wakati akizungumza kwenye
uzinduzi wa Tamasha la Mwanga Marathon and Festival-2024 ambalo limelenga kuvitangaza
vivutio vya utalii, kukuza uchumi wa wananchi wa wilaya hiyo na kuhamasisha
ushirikiano wa kijamii kupitia shughuli mbalimbali za kibiashara.
“Ninamshukuru na kumpongeza sana Mkurugenzi wa Kisangara Tours Ltd Frida Mberesero, kwa kazi kubwa ambayo umeifanya ya kuviibua na kuvionesha vivutio mbalimbali vya utalii vilivyopo wilaya hapa, ambavyo tutavitumia kama sehemu ya kuchochea utalii ndani ya wilaya yetu,”alisema DC Mnkunda.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa
Kisangara Tours Ltd, Frida Mberesero, aliwataka wananchi kufanya utalii wa
ndani ili kukuza kipato na Uchumi wa nchi huku
akiwaomba viongozi wa Serikali za Vijiji na Kata yaliko maeneo yenye
vivutio hivyo, yakiwemo maporomoko ya maji, kuhakikisha yanalindwa na kutunzwa.