Madaktari bingwa wa Dk.Samia waanza kutoa huduma za kibingwa Kilimanjaro

MOSHI-KILIMANJARO

Madaktari Bingwa na Bingwa Bobezi, kutoka hospitali ya rufaa ya Bombo-Tanga, Maunt Meru Jijini Arusha, Manyara, hospitali ya rufaa ya mkoa Mawenzi, KCMC, Benjamini Mkapa na hospitali ya rufani ya Taifa ya Magonjwa Ambukizi ya Kibong'oto (KIDH),wameanza kutoa huduma katika hospitali ya rufaa ya Mkoa Mawenzi ili kuwapunguzia ghalama kwa kufuata huduma hizo katika hospital kubwa nchini.

Hayo yamesemwa na Mganga Mfawidhi Hospitali ya Rufaa mkoa Mawenzi Dk. Edna-Joy-Munisi, wakati wa ufunguzi wa Kambi ya Madaktari Bingwa na Bingwa Bobezi wa Dk. Samia Kanda ya Kaskazini, na kusema kuwa tangu zoezi hilo lianze kufanyika Desemba 2 mwaka huu, wamefanikiwa kuona jumla ya wagonjwa 1,328 kati yao wagonjwa 22 tayari wamefanyiwa upasuaji.

“Ninawashukuru madaktari bingwa na bingwa bobezi waliopo hospitalini hapana waliotoka mikoa jirani kwa kukubali kuja kutoa huduma hizi hapa Kilimanjaro, najua ni jukumu zito lakini wamejitoa kuja kutuhudumia,”amesema Dk. Munisi.

Dk. Munisi amesema, wateja wengi wameendelea kujitokeza katika hospitali hiyo,huku wengi wao wakiwa ni wanawake  ambao wamekuwa wakifika kwa dakatari bingwa wa wanawake na uzazi, daktari wa magonjwa ya ndani, sanjari na daktari bingwa wa upasuaji.

Akizindua kambi ya madaktari bingwa mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Nurdin Babu, amesema serikali ya awamu ya sita imefanya mapinduzi makubwa katika sekta ya afya hapa nchini.

“Leo tunajionea mapinduzi makubwa katika hospitali zetu za rufaa za mikoa kwa kuwa na miundombinu, vifaa na vifaa tiba, na hivyo kuwezesha huduma za kibingwa na bingwa bobezi kutolea kama ambavyo leo hii katika hospitali yetu ya rufaa ya mkoa Mawenzi,”amesema.

Amesema maboresho hayo yanakwenda sanjari na kutoa ajira katika sekta ya afya, ambapo katika  hospitali ya mkoa Mawenzi imepokea waajiriwa wapya 64 wa kada mbalimbali.

Babu, amesema katika kuhakikisha huduma za afya zinaimarika kwa wananchi wake, serikali imekuwa na utaratibu wa kufanya huduma za Mkoba, kibingwa na bingwa bobezi, katika mikoa mbalimbali hapa nchini, ikilenga wananchi wapate huduma za afya ndani ya mikoa yao na kwa mkoa wa Kilimanjaro jumla ya huduma 19 zitatolewa na timu ya wataalam hao wa afya.

“Wale wote waliofika hapa kwa ajili ya changamoto mbalimbali za kiafya, watapata ufumbuzi na Mungu akipenda wataondoka hapa wakiwa wamepona kabisa na kuendelea na shughuli zao za kiuchumi,”amesema.

Amesema kuwepo kwa kwa madaktari hao bingwa na bingwa bobezi, ni moja ya fursa kwa wananchi kuweza kufikiwa na kupata huduma za afya bora na za kitaalamu.

Naye Mganga Mfawidhi hospitali ya Rufaa mkoa wa Tanga Dk. Frank Shega, amesema katika kuhakikisha huduma za afya kwa wananchi zinaimarika, uboreshaji wa miundombinu, vifaa tiba, mashine za vipimo,  

“Utaratibu wa kuwalipia madaktari bingwa kwa ajili ya kwenda kusomea ubobezi, umesaidia kuweza kurudi kwa jamii kwa ajili ya kuweza kuwasaidia kutoa huduma za afya kwa wananchi, badala ya wananchi kwenda katika hospitali za rufaa za Kanda au hospitali za rufa za Kitaifa.”amesema Dk. Shenga.

Mwenyekiti wa Bodi ya Ushsuri ya hospitali ya rufaa ya mkoa Mawenzi, Boniphace Clement Panga, amesema huduma za kibingwa wananchi walikuwa wakizifuata katika hospitali za rufaa, kutokana na serikali kuwa sikivu  imeamua  kuzisogeza karibu kule wanakotoka.

“Zoezi hili ni kumpunguzi mgonjwa gharama za kusafiri umbali mrefu kwa kufuata huduma hizo mbali na eneo wanakotoka,”amesema Panga.










Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.