Mkurugenzi Msaidizi
Rasilimali Watu Bi. Shani Kamala (kulia) akimkabidhi gari aina ya Land Cruzer Prado TXL Mkuu wa Chuo cha Viwanda vya Misitu FITI Moshi Dkt. Zacharia Lupala.
MOSHI-KILIMANJARO.
Katibu Mkuu Wizara ya
Maliasili na Utalii Dkt. Hassan Abbasi, amekabidhi gari kwa Mkuu wa Chuo cha
Viwanda vya Misitu (FITI) ikiwa nia hadi yake aliyoitoa Novemba 1,2024
alipokuwa mgeni rasimi katika mahafi ya 27 ya chuo hicho.
Akikabidhi gari hiyo kwa
niaba ya Katibu Mkuu, Mkurugenzi Msaidizi Rasilimali Watu Shani Kamala,
amekabidhi gari hilo Novemba 5, 2024 kwa mkuu huyo wa Chuo Dkt. Zacharia Lupala.
Kamala amesema Katibu Mkuu Dkt.
Hassan Abbasi, alimuahidi Mkuu wa Chuo cha Viwanda vya Misitu FITI Moshi, kumpatia
gari aina ya Land Cruzer Prado TXL yenye namba ya usajili STL 6702 na mimi ameniagiza
kwa niaba yake kuja kulikabidhi gari hili.” amesema.
Aidha Kamala amesema
kutolewa kwa gari hilo ni sehemu ya juhudi za Serikali ya Dkt. Samia Suluhu
Hassan za kuboresha utendaji kazi wa
taasisi hiyo.
Kwa upande wake Mkuu wa Chuo
hicho Dkt. Zacharia Lupala, amemshukuru Katibu Mkuu kwa kutoa gari hilo,
akieleza kwamba litamsaidia kuongeza ufanisi wa kazi katika majukumu yake.
“Nimetoka kupokea gari
ambalo Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii, alielekeza linunuliwe kwa
ajili ya ofisi ya mkuu wa chuo katika kuimarisha utendaji kazi wangu na gari
hiyo nimekabidhiwa leo,”amesema DKt. Lupala.
Amesema gari hiyo ataitumia
kwenye shughuli za utawala kaka ilivyokusudio lake katika kuboresha ufanisi na
utendaji kazi wa taasisi yake.
“Ninaishukuru sana Wizara
ya Maliasili na Utalii, kwa namna inavyotuongoza na kutuelekeza na kutusaidia
katika kutatua changamoto mbalimbali zinazotukabi na kuweza kutekeleza majukumu
yetu, ambayo tumekuwa tukiyafanya kila siku katika kutoa mafunzo ya viwanda vya
misitu Moshi.