Zimamoto yapiga marufuku vimiminika vinavyolipuka kuhifadhiwa ndani ya nyumba

MOSHI-KILIMANJARO

Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mkoani Kilimanjaro, limepiga marufuku wananchi ambao wamekuwa wakinunua vimiminika na kuhifadhi kwenye vidumu, kopo na kwenye chupa za plasiti, kisha kuhifadhi majumbani mwao, kuacha mara moja ili kupunguza majanga yanayotokana na moto.

Kauli hiyo imetolewa na Kaimu Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mkoa wa Kilimanjaro Mrakibu Jeremiah Mkomagi, wakati akiongea na waandishi wa habari kwenye kilele cha oparesheni ya mafunzo ya pamoja kati ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kutoka Jiji la Marburg Nchini Ujerumani.

Mkomangi amesema ni hatari kuwa na vimiminika vya moto ndani ya nyumba na kuwataka wananchi kuchukua tahadhari ili kuweza kuzuia majanga kama hayo yasiweze kutokea.

Aidha alisema Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mkoani humo, limefanya oparesheni ya pamoja kati ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kutoka Jiji la Marburg nchini Ujerumani.

Amesema ushirikiano huo umekuja baada ya kuingia makubaliano ya kimiji baina ya Manispaa ya Moshi na Ujeruni kwa kipindi cha miaka miwili.

Nao baadhi ya wanafunzi wa shule ya Sekondari ya Lucy Lameck, iliyoko Manispaa ya Moshi ambao wako katika Klabu ya kujitolea ya Jeshi la Zimamoto na Ukoaji Manispaa ya Moshi, walielezea namna walivyofundishwa kuhusu matumizi ya vifaa na mbinu mbalimbali za matumizi ya vifaa hivyo kama ambavyo wanaeleza.

Akizungumza Mganga mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Dkt. Jairy Khanga amesema ushirikiano huo baina ya Manispaa ya Moshi na Jiji la Marburg nchini Ujerumani, utaleta faida chanya, ikiwemo hospitali ya rufaa ya mkoa Mawenzi.


















 

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.