MOSHI-KILIMANJARO
Halmashauri ya Manispaa ya
Moshi, imepokea kiasi cha Sh Bilioni 1.8 kutoka Serikali Kuu kwa ajili ya ujenzi
wa Hospitali ya Wilaya ya ambayo inajengwa kwa majengo ya kwenda juu (ghorofa) eneo
la Msaranga Kata ya Ng’ambo ili kupambana na changamoto ya ufinyu wa eneo.
Hayo yamo kwenye taarifa ya
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi Mwajuma Nasombe, aliyoisoma Septemba 25,2024 kwa Kamati ya Siasa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) iliyotembelea na kujionea maendeleo
ya ujenzi wa hospital hiyo.
Mwl. Nasombe amesema katika mwaka wa
fedha 2021/2022 na 2022/2023 Halmashauri hiyo ilipokea kiasi cha Sh
Bilioni 1.8 kati ya fedha hizop kiasi cha Sh bilioni 1.2. zimekwisha kutumika na kwamba hatua ambayo inayoendelea
kwa sasa katika mradi huo ni kukamilisha slub kwa ghorofa ya chini na kusuka
nguzo kwa ajili ya ghorofa ya kwanza, ambapo hadi kukamilika kwake utagharimu kiasi cha Sh Bilioni 6.5
Akizungumza Mstahiki
Meya wa Manispaa ya Moshi Mhandisi Zuberi Kidumo, amesema lengo la Manispaa
kujenga hospitali ya Wilaya ilikuwa ni kupunguza msongamano wa wagonjwa katika
hospitali ya rufaa ya mkoa Mawenzi na kwenye hospitali ya Kanda ya Kaskazini KCMC.
“Tunaishukuru sana Serikali
kwa kuweza kutuletea fedha hizi kwa ajili ya ujenzi wa hospitali ndani ya Manispaa yetu, kukamilika kwa hospitali hii, itakwenda kutatua
changamoto za wananchi kuweza kupata huduma karibu na maeneo yao,”amesema
Mhandisi Kidumo.
Naye Mbunge wa Jimbo la Moshi
Mjini Priscus Tarimo, amesema “Serikali ilitutaka tuwe na heka 20 mpaka 50 ndipo iweze kutoa fedha za kujenga hospitali, kwa sasa hospitali inapojengwa ni eneo lenye heka sita tu, naishukuru sana Serikali kwa
kukubali kutoa fedha za kujenga hospitali hii kwa ghorofa,”amesema Tarimo.
Ameongeza kusema “Ni kweli
kabisa Serikali kama ingeweza kusimia miongoza ya Wizara ya Afya kama inavyotaka,
leo hii tusingeweza kupata fedha za kujenga hospitali kwenye eneo lenye heka
sita.”
Kwa upande wake Mwenyekiti
wa CCM Mkoa wa Kilimanjaro Patrick Boisafi ampongeza Mbunge Priscus Tarimo, kwa
ushawishi wake mkubwa Bungeni na kuweza kufanikisha kujenga hoja Serikalini na
ikakubali kutoa fedha kwa ajili ya kujengwa kwa hospitali hiyo.
“Ni kweli mkoa wetu wa Kilimanjaro
tuna changamoto ya ufinyu wa ardhi, Kamati ya Siasa ya mkoa inakupongeza sana Mbunge kwa kutengeneza
ushawishi, wakaielewa hoja yako, wakakuunga mkono na ndio maana Serikali imetenga
Sh bilioni 6.5 kwa ajili ya ujenzi wa hospitali hii”.







